Header Ads

ad

Breaking News

General Motors imerudi tena katika soko la Tanzania ikiwa imeongeza ufanisi zaidi

????????????????????????????????????
Kutoka kulia ni Mwenyekiti  wa Kampuni ya QAM Bw, Yusuf Manji, Hiroyuta Kubota kutoka Ubalozi wa Japan Nchini Tanzania, Toru Nakata Ofisa Mtendaji Mkuu Kutoka Isuzu na Mario Spangeberg Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa GM Africa kutoka Afrika Kusini wakikata utepe kuzindua Show Room kubwa na kuuza magari ya Isuzu na Chevrolet na bidhaa zake hapa nchini katika uzinduzi uliofanyika kwenye jengo la Quality Group Barabara ya Nyerere jijini Dar es salaam jana. 
????????????????????????????????????
 Viongozi hao wakiangalia ngoma za utamaduzi zilizokuwa zikitumbuizwa katika uzinduzi huo.
Baadhi ya magari yakionyeshwa katika Show Room hiyo.


Baadhi ya magari yakionyeshwa katika Show Room hiyo.

????????????????????????????????????
Baadhi ya wageni mbalimbali wakiwa katika uzinduzi huo.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
………………………………………………………………………………..
Wenya magari Tanzania leo wana sababu ya kutabasamu maana Kampuni ya magari ya General Motors East Africa (GMEA) Limited  wamesaini makubaliano ya kibiashara na Quality Automotive Mechanization Limited (QAML) ambayo itashuhudia  kampuni ya magari ikiingia kwenye soko la Tanzania.
Kupitia uuzaji mpya, wateja wa General Motors wataweza kununua bidhaa mpya aina ya Isuzu na Chevrolet kutoka katika sehemu za mauzo huku wakipata huduma za kimataifa kutoka katika eneo maalumu la magari hayo.
Akizungumza hi leo wakati wa sherehe ya kutia saini makubaliano ya biashara, Mwenyekiti  wa Kampuni ya QAM Bw, Yusuf Manji aliahidi wateja ngazi bora ya urahisi na faraja .
 “Tumeweka uwekezaji mkubwa na muhimu kuhakikisha mafanikio ya kituo hiki na kuwezesha kupenya kwa haraka kwa bidhaa za Isuzu na Chevrolet katika soko hili lenye ushindani mkubwa”. Alisema
Eneo la mauzo ya magari limetengenezwa ili kutoa na kuwapatia wateja uzoefu na uimara kwa ujumla na bidhaa za General Motors, pamoja na kutoa huduma za mauzo na vifaa vya magari.
Mkurugenzi mtendaji wa GMEA Bi. Rita Kavashe alisema Kampuni ya General motors kuingia katika soko la Tanzania ilikuwa ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu katika kampuni hiyo ili kuimarisha uwepo wake katika Afrika Mashariki.
“Tanzania imejitokeza katika soko na kama General Motors tulitaka kuwa sehemu ya ukuaji huu. Sehemu hii ya mauzo itakuwa ni hatua ya kuingia kwa bidhaa zetu zenye ubora na zimetumia utaalamu mkubwa katika utengenezwaji wake  ambapo tunatanua wigo wetu katika ukanda huu. Kupitia uuzaji huu, wateja wetu watanunua aina mpya za Chevrolet na Isuzu huku wakipata huduma bora”.Alisema
Bi. Kavashe alisema kuingia ndani ya soko la Tanzania imetokana na kukua kwa kasi kwa biashara ndani ya ukanda wa Afrika Mashariki hasa katika kuendeleza ushirikiano wa masoko ya umoja. Soko la jumuia ya Afrika Mashariki lina takribani watu milioni 140 .
“Tanzania ni soko linalokua kwa kiwango kikubwa na imekua ni soko muhimu tunalolitazamia tunapotafuta kujikita katika soko lenye watu wengi na idadi inayokua kila kukicha. Ukuaji wa viwanda na
kuongezeka kwa kipato ili kutengeneza ongezeko la watu wa tabaka la kati katika nchi hii ina maana kuwa kuna soko changa la bidhaa zetu, “aliongezea Kavashe.

No comments