Header Ads

ad

Breaking News

Banza Stone ametutoa, pengo katika muziki

Mwanamuziki nyota wa muziki wa dansi, Ramadhani Masanja 'Banza Stone', amefariki dunia.
Banza amefariki dunia alipokuwa amelazwa katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam. 
Ramadhan Masanja 'Banza Stone'


 
Mwanamuziki huyo aliyetamba akiwa na bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' na Tanzania One Theatre (TOT), alikuwa amelazwa hospitalini kwa muda mrefu.

Mkurugenzi wa bendi ya Twanga Pepeta, Asha Baraka, amethibitisha kifo cha Banza Stone baada ya kupigiwa simu.

“Ni kweli Banza amefariki leo saa saba, tumepata taarifa hizo za msiba, tunasikitika sana kwani alikuwa na mchango mkubwa katika tasnia ya muziki,” alisema Asha Baraka.

Katika siku za hivi karibuni, Banza amekuwa akizushiwa kifo kupitia mitandao ya kijamii na vyombo mbalimbali vya habari. Tunamwomba Mungu aipumzishe roho ya Banza Stone mahali pema peponi. Amina

No comments