Header Ads

ad

Breaking News

Yanga yaishusha Azam FC, yaichapa JKT Oljoro


Yanga

 Na Mwandishi Wetu, Arusha

BAO pakee lililofungwa na beki wa Yanga, Mbuyu Twite dhidi ya Oljoro JKT ya mjini hapa leo,  limeiwezesha timu yake hiyo kuchupa hadi nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara na hivyo kuiporomosha Azam iliyokuwa ikishika nafasi hiyo kwa muda mrefu sasa.

Matokeo hayo yameiwezesha Yanga kufikisha pointi 20 kutokana na mechi 10, ikiwa nyuma ya Simba inayoshikilia usukani kwa kwa pointi zao 22, timu zote hizo zikwia zimeshuka dimbani mara 10.

Azam iliyopokea kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Simba kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jana, imebakiwa na pointi zake 18 na sasa inashika nafasi ya tatu katika ligi hiyo inayojumuisha timu 14.

Katika mchezo huo wa jana uliopigwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, mjini hapa, Yanga iliuanza kwa kasi ya wastani ambapo washambuliaji wake walipata nafasi kadhaa za kufunga ambazo hata hivyo walishindwa kuzitumia vema.

Kwa upande wao, JKT Oljoro wanaonolewa na kipa wa zamani wa Yanga, Mbwana Makata, walionyesha upinzani wa aina yake kwa mabingwa hao wa Afrika Mashariki na Kati na kwamba iwapo wangekuwa makini, wangeweza kupata bao la mapema kama washambuliaji wake wangekuwa makini.

Kwa ujumla, mchezo huo ulitoa burudani ya nguvu kwa wapenzi wa soka wa jijini hapa waliojitokeza kwa wingi kuwaona nyota wa Yanga, hasa waliosajiliwa msimu huu.

Miongoni mwa nyota waliokuwa kivutio uwanjani hapo, ni Twite na Didier Kavumbagu ambapo mashabiki wa soka wa hapa walionekana kuwasogelea kutaka kuwaona kwa karibu zaidi.

Katika mechi nyingine iliyochezwa kwenye Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani, timu ya Ruvu Shooting, jana ilitumia vema uwanja wake wa nyumbani baada ya kuichapa Polisi Morogoro mabao 2-1.
Polisi Moro walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Malimi Busungu dakika ya 66, lakini Ruvu Shooting walisawazisha dakika ya Shaban Suza dakika ya 69, kabla ya Said Dilunga kuihakikisha timu ushindi kwa kuifungia bao la pili dakika ya 77.

No comments