Okwi namba nyingine Simba, aonesha kiwango
Okwi |
*Azam FC yapigwa 3-1, kama wamelala
Na Mwandishi Wetu
MABINGWA wa
Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba, wamezidi kujikita kileleni mwa ligi hiyo baada
ya leo, kuikandamiza Azam mabao 3-1 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, huku
nyota wake, Emmanuel Okwi, Shomary Kapombe, Felix Sunzu na Mrisho Ngassa
waking’ara vilivyo.
Kwa matokeo
hayo, Simba wamefikisha pointi 22, huku Azam wakibakiwa na pointi zao 18 na
hivyo kuporomoka hadi nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi hiyo, baada ya
Yanga kuichapa JKT Oljoro bao 1-0 kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid na kuipoka
Azam nafasi ya pili.
Katika
mchezo huo wa jana, Azam ndio walioanza kupata bao lililofungwa na John Bocco
katika dakika ya nne baada ya kupokea pasi ya Salum Abubakari na kuwafungasha
mabeki wa Simba, Paschal Ochieng na Shomari Kapombe kutoka katikati ya uwanja
na kumchambua vilivyo kipa wa Simba, Juma Kaseja kuipa timu yake bao la kwanza.
Bao hilo
liliwazindua Simba na kujipanga kufanya mashambulizi ya nguvu na hatimaye
kusawazisha dakika tatu baadaye kupitia Mzambia Felix Sunzu aliyeunganisha kwa
kichwa krosi ya Said Nassor ‘Chollo’.
Katika
dakika ya 40, Emmanuel Okwi aliifungia Simba bao la pili kwa kichwa,
akiunganisha vema krosi ya kiungo Mwinyi Kazimoto kutoka wingi ya kushoto.
Okwi
aliifungia Simba bao la pili dakika ya 51, akipiga kiufundi mno mpira uliotinga
moja kwa moja nyavuni akiwa nje kidogo ya 18.
Baada ya
mabao hayo, Simba walionekana kucharuka zaidi na kuichezesha mchakamchaka Azam
kadri walivyotaka, ambapo Okwi, Ngassa, Sunzu na beki Shomari Kapombe
waling’ara mno.
Dakika ya
17, Kazimoto alipiga shuti kali akiwa nje kidogo ya 18, lakini shuti hilo
lilitoka nje kidogo ya lango la Azam.
Hamis Mcha
aliyeingia uwanjani kuchukua nafasi ya Bocco aliyeumia, aliikosesha Azam bao
baada ya kushindwa kutulia akiwa ndani ya sita ya lango la Simba ambapo alipiga
fyongo iliyookolewa na Kaseja.
Iwapo
mchezaji huyo angekuwa makini, angempasia Kipre Tchetche aliyekuwa katika
nafasi nzuri ya kufunga, lakini alilazimisha kufunga akiwa katika pembe ya goli
na kushindwa kufanya hivyo.
Okwi nusura
afunge bao katika dakika ya 35 ambapo shuti lake akiwa pembeni ya lango la
Azam, liligonga mwamba na mpira kumkuta Mrisho Ngassa aliyepiga shuti kali
lililowababatiza mabeki wa wapinzani wao hao.
Kazimoto
alikosa bao la wazi katika dakika ya 46 akiwa ndani ya 18 ambapo shuti lake
lililotokana na pasi maridadi ya Okwi, lilidakwa na kipa wa Azam, Mwadini Ally.
Dakika ya
79, Ochieng aliokoa bao la wazi la Azam kutokana na mpira wa kichwa uliopigwa
na Kipre na kuokolewa na beki huyo katika mstari wa goli.
Simba: Juma
Kaseja, Said Nassor ‘Chollo’, Amir Maftah, Shomari Kapombe, Paschal Ochieng,
Jonas Mkude, Mwinyi Kazimoto, Amri Kiemba/Ramadhan Chombo ‘Redondo’, Felix Sunzu/Ramadhan
Singano ‘Messi’, Emmanuel Okwi na Mrisho Ngassa/Christopher Edward.
Azam:
Mwadini Ally, Ibrahim Shikanda, Sahm Nuru, Said Morad, Agrey Morris, Addulhalim
Humoud, Jabir Aziz/Bolou Michael, Himid Mao/Abdu Kassim ‘Babi’, John
Bocco/Hamis Mcha, Kipre Tchetche na Salum Abubakar.
No comments