Header Ads

ad

Breaking News

Simba yateswa na mechi za ugenini

Kikosi cha Simba

Na Mwandishi Wetu, Morogoro

TIMU ya soka ya Polisi Morogoro, jana ilifanikiwa kuibana Simba, na kutoka nayo sare ya bao 1-1, katika mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara iliyochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Polisi Moro iliyopo mkiani mwa ligi hiyo, ilianza mchezo huo kwa kasi na kufanya mashambulizi langoni mwa  Simba, lakini safu ya ulinzi ya wapinzani wao iliyokuwa chini ya Mkenya Pascal Ochieng, ilikuwa imara kuhakikisha nyavu zao hazitikiswi.

Mashambuliji ya maafande wa Polisi Moro, yalizaa matunda dakika ya 33, baada ya Mokili Lambos kuifungia timu yake bao.

Lambo  aliyetokea kwenye benchi kuchukua nafasi ya John Bosco, aliukwamisha mpira huo  wavuni, baada ya kuubetua kiufundi mpira wa krosi uliopigwa kutoka upande wa kulia na kumpita kipa Juma Kaseja Juma .

Kufungwa kwa bao hilo kuliwafanya Simba watulie na kucheza soka zuri la kiufundi, lakini washambuliaji wake, Emanuel Okwi, Felix Sunzu, Mrisho Khalfan Ngasa na Amri Kiemba, walishindwa kusawazisha bao hilo dakika 45 za kwanza za mchezo huo.  

Simba walikianza kipindi cha pili kwa kulisakama lango la Polisi, huku wakionana vizuri na kuwachanganya mabeki wa wapinzani wao, kabla ya mpira wa kona uliopigwa na Emmanuel Okwi ulitua kwa Amri Kieemba ambaye hakufanya makosa, kwa kuukwamisha wavuni dakika ya 57.

Kwa matokeo hayo, Simba imefikisha pointi 23, ikiwa na sawa na Yanga, ambao jana waliibuka na ushindi wa mabao 3-0, dhidi ya Mgambo JKT, mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
ciao

No comments