Header Ads

ad

Breaking News

TASWA yampongeza Wambura, Mkutano mkuu waiva


Katibu Mkuu TASWA

Na Mwanadishi Wetu
 CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), kimepongeza mwanachama wake Boniface Wambura, kwa kuteuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu la Afrika (CAF) kuwa mmoja wa maofisa watakaoshughulikia masuala ya habari wakati wa fainali za Mataifa ya Afrika kwa Wanawake zitakazofanyika nchini Equatorial Guinea.
 Katika taarifa iliyosambazwa leo na chama hicho, kupitia Katibu Mkuu wake, Amir Muhando, alisema wamepokea kwa furaha uteuzi huo wa Wambura ambaye ni Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na inaamini ataendelea kufanya vizuri kama anavyotekeleza majukumu yake ya kazi ndani ya TFF.
 “Katika hili waandishi wa habari za michezo nchini ni mashahidi wa hilo kwani amekuwa mtu sahihi kwao na amekuwa na ushirikiano mkubwa usio na kifani kwa wanahabari wenzake.
 “Kwa vile Wambura ni mwanachama wetu hai wa TASWA, kwa kuteuliwa kwake huko ni faraja kwa chama na tunamtakia kila la heri ili aweze kutekeleza vyema majukumu yake kwani hiyo ni ishara tosha kwamba kazi yake inaonekana na inathamanika,” alisema.
 Uteuzi wa Wambura, umefanywa na Rais wa CAF, Issa Hayatou kwa ajili ya kufanikisha uendeshaji wa fainali hizo za Mataifa ya Afrika kwa Wanawake zilizopangwa kuanza Oktoba 28 mpaka Novemba 11, mwaka huu.
 Wengine walioteuliwa ni ofisa kutoka Makao Makuu ya CAF, Mahmoud Garga na Arlindo Macedo kutoka Angola.

… Mkutano mkuu wanukia

Na Mwandishi Wetu

SSKRETARIETI ya Chama cha Waaandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), imefikia hatua ya mwisho ya mazungumzo na mdhamini wa Mkutano Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao katika tarehe ambayo itatangazwa rasmi.
 Kamati ya Utendaji ya TASWA, ilikubaliana katika kikao chake mwezi uliopita kuwa Mkutano Mkuu wa TASWA mwaka huu uwe wa aina yake kwa kuwawezesha wanachama kukaa pamoja na kubadilishana mawazo na ikashauri ikiwezekana ufanyike nje ya Dar es Salaam kama hali itaruhusu.
 Kutokana na hali hiyo, kikao kiliiagiza sekretarieti ya TASWA itafute mdhamini wa kufanikisha suala hilo na kwamba kama ikishindikana mkoani ifanyike Dar es Salaam lakini kuwe na mdhamini.
 “Tayari hilo limefanyika na mdhamini amepatikana, ambapo hatua ya mwisho ya mazungumzo na mdhamini itakuwa mapema wiki ijayo  na baada ya hapo itatangazwa tarehe rasmi.
 “Nichukue nafasi hii kuwaomba wanachama ambao hawajalipa ada zao wafanye hivyo kwa kuwasiliana na Mhazini wa chama au Mhazini Msaidizi ili waepuke usumbufu wa kushindwa kuhudhuria mkutano huo,” alisema Mhando.

No comments