Header Ads

ad

Breaking News

Tanzania Prisons wapata ajali wakielekea kuivaa Magombo Tanga


Prisons

 Na Mwandishi Wetu

WACHEZAJI sita wa timu ya soka ya Tanzania Prisons ya Mbeya inayoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, jana ilipata ajali maeneo ya Segera na Hale mkoani Tanga, wakati wakielekea jijini Tanga kucheza na Mgambo Shooting.

Akizungumza na SuperStar kwa njia ya simu jana, Kocha mkuu wa timu hiyo, Jumanne Challe, alisema kuwa, wachezaji 16 waliumia katika ajali hiyo, ambapo sita wamelazwa katika hospitali ya Muheza.
Aliwataja wachezaji waliolazwa ni David Mwantika, Lugano Mwagama, David Mwasongwe, Sino Agustino, Halid Fungambeck na Sadick Jumbe.

“Tulipata ajali mbaya jana (juzi) maeneo ya Segera na Hale, tukiwa njiani kwenda Tanga, kama si dereva wetu kukwepa, tungekufa wote, maana tungegongana uso kwa uso, lakini alifanikiwa kulikwepa na tukapinduka mara tatu.

“Wengine si wazima sana, wengi wao wameumia mbavu, shingo, magoti, migongo viuno, na hata mimi niliumia mguu wa kushoto,” alisema Challe.

Kocha huyo alisema kwamba, daktari wa timu hiyo anaandaa ripoti ya wachezaji, na ikikamilika, wataipeleka kwa msimamizi wa kituo ili aweze kuiwasilisha katika ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

No comments