Header Ads

ad

Breaking News

Simba, Yanga kibaruani kesho




LIGI Kuu Tanzani Bara, inatarajia kuendelea tena hii kesho, ambapo Mabingwa wa ligi hiyo Simba na Yanga watashuka dimbani.

Simba watakuwa wenyeji wa Azam FC kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, wakati Yanga watakuwa ugenini kucheza na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa kumbukumbu wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha.

Masikio ya mashabiki wa soka hapa Tanzania yatakuwa kwenye viwanja vyote viwili kutokana na upinzani wa pointi uliopo kwa timu tatu Simba, Yanga na Azam FC.

Hadi leo, Simba inaongoza kwa pointi 19 wakiwa wamecheza mechi tisa sawa na Yanga mwenye pointi 17, Azam ikiwa nafasi ya pili 18 na mchezo mmoja mkononi.

Kutokana na matokeo hayo kazi kubwa itakuwa kwa Simba na Azam ambao wanakutana kila mmoja akitaka ponti hizo tatu ili kuweza kusonga mbele.

Yanga tayari wamewasili jijini Arusha juzi, huku wachezaji wakiwa wenye furaha baada kupewa fedha kwa ajili ya kuwapa morali katika mchezo wa kesho.

Ili wawapite wapinzani wao Simba na Azam wanatakiwa kushinda mchezo wa leo huku wakisikilizia matokeo ya wapinzani wao na siyo kutoa sare. 

Huko Msimbazi, nako mambo siyo shwari kutokana na mpasuko uliopo kati ya viongozi na wachezaji, leo watakuwa na kibarua kigumu kuhakikisha wanashinda ili mambo yakae sawa.

Timu ya Simba iliweka kambi visiwani Zanzibar kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa kesho baada ya kupoteza pointi sita kwa kutoka sare mara tatu mfululizo.

Azam wao bado wanatakiwa kushinda na hata kama wakitoka sare bado ana faida ya mchezo mmoja mkononi.
Mbali na mechi hizo, African Lyon itakuwa mwenyeji wa Kagera Sugar katika Uwanja wa Chamazi huku Ruvu Shooting ikiikaribisha Polisi Moro Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani.

No comments