Header Ads

ad

Breaking News

Benzema akubali mambo ya Mourinho


Jose Mourinho

MADRID, Hispania
 Karim Benzema amesisitiza kuwa, ataendelea kuitumikia klabu yake ya Real Madrid inayocheza ligi kuu ya Hispania ‘La Liga’.
 Mshambuliaji huyo kutoka Ufaransa, amekuwa akihusishwa kuondoka wakati wa usajili wa dirisha dogo la Januari mwakani, baada ya Real kumtupia macho mshambuliaji wa Atletico Madrid, Radamel Falcao. 
 "Kocha ananiamini sana na tunafanya kazi nzuri kutokana na imani yake kwangu. Na sasa nimeiva katika kila kitu. Nilikuwa na mambo mengi yakipanda na kushuka tangu nilipotua Madrid, lakini bado nipo hapa. 

"Jose Mourinho, ni bonge la kocha na anatuunga mkono. Hofu ni sehemu ya maisha yangu tangu nilipokuwa Lyon, lakini hapa ni zaidi kwani nipo katika klabu bora duniani."

No comments