Header Ads

ad

Breaking News

Messi ni bora anastahili Ballon d'Or- Vilanova


Lionel Messi

 BARCELONA, Hispania
KOCHA wa Barcelona, Tito Vilanova, amezidi kumpa nafasi kubwa Lionel Messi, kubeba uchezaji bora ‘Ballon d'Or’. 

Messi, alifunga mabao matatu ‘hat-trick’, katika mechi dhidi ya Deportivo La Coruna ya ligi kuu Hispania na kuisaidia timu yake kuibuka na ushindi mnono. 

“Hastahili kwa sababu ya kile alichokifanya siku iliyopita, lakini anastahili kwa sababu ya yale aliyofanya kwa mwaka mzima,” alisema Vilanova. 

Vilanova aleweka wazi kuwa, hamfanyii kampeni Messi, lakini ni kwamba, “hakuna mchezaji atakayefanya kile alichokifanya Messi.”

No comments