Header Ads

ad

Breaking News

AZAM, RUVU SHOOTING BAO 1-1




Na Mwandishi Wetu, Chamazi

TIMU za Azam FC na Ruvu Shootin, leo zimetoshana nguvu baada ya kutoka sare ya bao 1-1, katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi jijini Dar es Salaam.

Katika mechi hiyo ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Ruvu Shooting walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Seif Abdallah.

hata hivyo, wakiwa bado wana furaha, waliumizwa na mshambuliaji wa kimataifa wa kutoka Ivory Coast, Kipre Tchetche, bao lililozifanya timu hizo kugawana pointi.

No comments