Header Ads

ad

Breaking News

Man Utd, Barcelona safi Ulaya, Chelsea mambo magumu



Manchester United wakishangilia bao
 LONDON, England

RAUNDI ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya iliyoanza Machi mwaka huu, ilihitimishwa jana usiku, huku kukiwa na matokeo ya kushangaza katika mechi za juzi usiku.

Manchester United ikicheza kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Old Trafford, jijini London, England, ilitoka nyuma na kushinda mabao 3-2 dhidi ya Sporting Braga 3-2, shukrani zikienda kwa Javier Hernandez aliyefunga mara mbili.

Alan aliifungia timu yake ya Ureno mara mbili kuipa uongozi wa mabao 2-0 hadi dakika ya 20, kabla ya Chicharito kubadili matokeo kuwa 2-1 dakika tano baadaye na Jonny Evans aliongeza la pili katika kipindi cha pili.

Mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Chelsea, walifungwa mabao 2-1 na Shakhtar Donetsk ya Ukraine kwenye Uwanja wa Donbass Arena kwa mabao ya Alex Teixeira na Fernandinhola kabla ya bao la kufutia machozi lililofungwa na Oscar dakika za mwisho.

Mabingwa wa Scotland, Celtic waliikamata Barcelona kwenye Uwanja wa Nou Camp, lakini bao la dakika za mwisho la Jordi Alba, liliwezesha miamba ya Catalan kupata ushindi wa mabao 2-1 baada ya Andres Iniesta kusawazisha bao la kuongoza la Giorgios Samaras dakika ya 18.

Kwingineko, Spartak Moscow iliifunga Benfica mabao 2-1, ikiwa ni baada ya Jardel kujifunga, wakati Juventus ilitoka sare ya bao 1-1 na Nordsjaelland ya Denmark, wakati Roberto Soldado alifunga mabao matatu ‘hat-trick’ kuiwezesha Valencia kuichapa BATE Borisov mabao 3-0.

Katika mchezo mwingine, penalti iliyofungwa na Thomas Muller, iliiwezesha Bayern Munich kuichapa Lille bao 1-0 na CFR Cluj iliibana Galatasaray na kutoka nayo sare ya bao 1-1 mjini Istanbul, Uturuki.

Matokeo ya mechi za juzi kwa ufupi
 KUNDI E
 Shakhtar Donetsk        2-1 Chelsea
Nordsjaelland               1-1 Juventus
  KUNDI F
 BATE Borisov   0-3 Valencia
Lille                     0-1  Bayern Munich
  KUNDI G
 Spartak Moscow          2-1 Benfica
Barcelona            2-1
 KUNDI H
 Manchester United      3-2 Sporting Braga
Galatasaray                   1-1 CFR Cluj-Napoca

No comments