Header Ads

ad

Breaking News

Bolt afanya maajabu, avunja rekodi yake


 Usain Bolt akimaliza mshindi wa mita 100 olimpiki.


LONDON, England

"Kuna watu wengi walisema siwezi kushinda hapa, kulikuwa na mengi pia yalisemwa. Ni hisia za aina yake kuona nimeyashinda yote hayo na kuthibitisha kuwa bado mimi ni namba moja na bado mimi ni bora"

BINGWA mara nne wa Olimpiki, Usain Bolt wa Jamaica, amesema anakaribia kuwa nguli wa mchezo huo duniani, baada ya Jumapili kutetea vema dhahabu yake ya fainali za Olimpiki katika mbio za mita 100.

Bolt (25), alishinda kwa muda wa rekodi akitumia sekunde 9.63 na sasa yu tayari kufanya tafakuri sahihi za kutetea na medali ya mita 20, jijini London.
"Dhahabu hii inamaanisha kuwa niko hatua moja tu kuelekea kuwa nguli wa mchezo huu, hivyo natakiwa kufanya kazi ngumu na ya ziada kufanikisha hilo,” alisema na kuongeza: "Kwamba niko hatua moja tu kabla.

"Naelekea kukimbia mita 200 sasa, hivyo napaswa kuangalia mbele kuona namna navyoweza kufanikisha hilo."

Bolt anapewa nafasi kubwa ya kuibuka na dhahabu ya mita 200, tukio ambalo pia alitwaa ushindi wa kwanza katika Olimpiki iliyopita jijini Beijing mwaka 2008. 

Muda wake wa sekunde 19.19, aliotumia katika mashindano ya ubingwa wa Dunia mwaka 2009 jijini Berlin, Ujerumani, bado unashikilia rekodi ya dunia ya kasi.
Alipoulizwa na BBC Radio 5 kama alikuwa akifikiria kushinda mchakato huo wa juzi, Bolt huku akitabasamu alisema: 

“Hasa, ilikuwa katika mawazo yangu kwa miaka kadhaa sasa na ukifuatilia nilichofanya msimu huu, utaona namna nilivyokuwa najiamini zaidi.

"Sitaki kusema naweza kufanya hivyo na kisha nikashindwa kufanya hivyo. Lakini inabaki mawazoni mwangu tu kuwa nataka kufanya hivyo, ndivyo ilivyokuwa pia."
"Kuna watu wengi walisema siwezi kushinda hapa," alisema Bolt. 

"Kulikuwa na mengi pia yalisemwa. Ni hisia za aina yake kuona nimeyashinda yote hayo na kuuonesha ulimwengu kuwa bado mimi ni namba moja nab ado mimi ni bora."

Bolt atakuwa sehemu ya wakali watakaonza mbio za mita 200 kwenye Uwanja wa Olimpiki jijini London leo huku fainali ikitarajiwa kufanyika hapo Alhamisi.

No comments