Rio: Mkenya Vivian Cheruiyot ashinda dhahabu

RIO DE JENEIRO, Brazil
Mkenya Vivian Cheruiyot ameshinda dhahabu katika mbioa za mita 5000 za akina dada mjini Rio, na kuweka rekodi mpya ya mbio hizo kwa muda wa dakika 14 sekunde 26.17.
Nafasi ya pili nayo
ilichukuliwa na mkenya mwanzake Hellen Obiri, ambaye alijishindia medali
ya fedha kwa muda wa dakika 14 sekunde 29.77
Muithiopia Almaz
Ayana ambaye alishinda dhahabu katika mbio za mita 10,000, alichukua
nafasi ya tatu kwa muda wa dakika 14 sekunde 42.89.
Cheruiyot sasa amepata medali mbili baada ya kupata fedha katika mbio za mita 10,000.
No comments