Header Ads

ad

Breaking News

Tanzania yabeba medali 11 michuano ya SARPCCO Swaziland

sa1
Wanariadha wa Tanzania walioshiriki michezo ya majeshi ya Polisi kwa nchi za Kusini mwa Afrika(SARPCCO) katika mji wa Mbabane nchini Swaziland wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza michezo hiyo.(Picha na Frank Geofray wa Jeshi la Polisi-Swaziland)
sa2
Wanariadha wa mbio za nyika (KM 10)  kutoka Polisi Tanzania wakifurahia baada ya kuvalishwa medali ya ushindi wa jumla katika mbio hizo wakati sherehe za kufunga michezo ya majeshi ya Polisi kwa nchi za Kusini mwa Afrika(SARPCCO) katika mji wa Mbabane Swaziland.(Picha na Frank Geofray wa Jeshi la Polisi-Swaziland)
………………………………………………………………………………..
Na. Frank Geofray-Jeshi la Polisi,Swaziland.
Timu ya wanariadha wa Polisi Tanzania waliokuwa wakishiriki michezo ya majeshi ya Polisi kwa nchi za Kusini (SARPCCO) nchini Swaziland imefanikiwa kumaliza michezo hiyo, huku ikipata jumla ya medali kumi na moja na hivyo kufanikiwa kushika nafasi ya tatu katika mchezo wa riadha.
Timu hiyo imefanikiwa kupata medali sita za dhahabu, tatue za fedha na mbili za shaba kutokana na wanariadha wake kumi na mbili walioshiriki michezo hiyo iliyoshirikisha jumla ya nchi kumi na tatu huku nafasi ya kwanza ikichukuliwa na Zimbabwe ikifuatiwa na Namibia.
Michezo hiyo ilifungwa jana na Waziri wa Katiba na sheria wa Nchi ya Swaziland Mhe.Seneta Hillary ambapo katika hotuba yake alisisitiza umoja na ushirikiano kupitia michezo kwa nchi wanachama wa umoja huo pamoja na kuzipongeza nchi zote zilizoshiriki na kuleta ushindani mkubwa.
Hillary alisema michezo hiyo imekuwa fursa kubwa ya kuwakutanisha wanamichezo wa majeshi ya Polisi hivyo amewaomba wakuu wa majeshi ya Polisi na nchi wanachama kuyapa umuhimu na kipaumbele michezo hiyo ili kuwawezesha askari polisi kubadilishana mbinu za kukabiliana na uhalifu pamoja na kujenga afya zao.
Akizungumzia matokeo hayo, Mkuu wa Kitengo cha Michezo wa Jeshi la Polisi, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi SSP Jonas Mahanga amesema michezo hiyo ilikuwa na ushindani mkubwa lakini timu ya Tanzania ilijitahidi na kujituma hivyo kufanikiwa kufanya vizuri ukilinganisha na timu nyingine zilizoshiriki micvhezo hiyo.
“Nawapongeza wachezaji wetu wa Tanzania wote kwa kazi nzuri waliyofanya hivyo kurejea na ushindi wa medali kumi na moja nyumbani na katika michezo mingine tunaendelea kujipanga vyema ili kufanya vizuri zaidi”Alisema Mahanga.
Timu hiyo inatarajia kurejea Tanzania siku ya Jumanne jioni kwa ndege ya shirika la Afrika kusini.

No comments