Header Ads

ad

Breaking News

Lowassa atikisa mkoani Mbeya

 

 Mgombea urais kupitia vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya wanchi (UKAWA), Edward Lowassa,akaiangalia bila kuamini idadi kubwa ya wananchi waliojitokeza kumsikiliza baada ya kufanya ziara ya kusaka wadhamini kwa mikoa ya Nyanda za juu kusini, hapo ilikuwa kabla ya kuwahutubia wananchi waliojitokeza kwa wingi katika viwanja vya Luanda Nzovwe, Jijini Mbeya Jana.
 ......................................................................................................................................................
Mgombea urais kupitia vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya wanchi (Ukawa), Edward Lowassa, amasema endapo atachaguliwa kuwa Rais hatakuwa na mchezo na watu wasiopenda maendeleo na kwamba ameahidi kubadili utaratibu wa utendaji kazi nchini ka watu kufanya kazi kwa saa 24, tofauti na ilivyosasa kwani hali hiyo inafanya uchumi wan chi kutochangamka.
 
Aliyasema hayo jana Jijini hapa alipofanya ziara ya kutafuta wadhamini kwa mikoa ya nyanda za juu kusini, ambapo baada ya kukabidhiwa orodha ya wadhamini alihutubia maelufu ya wakazi wa Mbeya, katika viwanja vya Luanda Nzovwe.
 
Lowassa aliyeanndamana na mkewe na mgombea Mwenza Juma Dun Haji, pamoja na viongozi mbalimbali wa UKAWA , pia alisema kazi nyingine atakayoifanya baada ya kuingia madarakani ni kuugeuza mkoa wa Mbeya kuwa mji wa Kimataifa na bakuwa kitovu cha uchumi unaosisimka kama ilivyo baadhi ya miji maarufu ya Ulaya.
 
“Nataka niwaambie niataubadilisha mji wa Mbeya kuwa wa kimataifa , kuwa kama  Nairobi na Uswis kwa kutumia zaidi uwanja wa kimataifa wa Songwe, Mbeya mji wenye uchumi wa kisasa” alisema Lowassa.
 
Mbali na ahadi hiyo kwa Mkoa wa Mbeya, Lowassa aliendelea kuwapaa matumani wananchi kwa kusema kuwa, akifanikiwa kushika dola ataunda serikali rafiki na wananchi wa kipato cha chini kama wamachinga, Bodaboda na Mama ntilie.
 
Lowasa pia alisema akiwa madarakni atamwachia mwanamziki maarufu aliyefungwa jela maisha kwa kosa la ubakaji, pamoja na familia yake< nguza Vicking (Babu Seya).
 
Alilazimika kutoa ahadi hiyo baada ya wananchi kuhoji juu ya mwanamziki huyo, ambapo wakati Lowassa akiaga baada ya kueleza mambo atakayoshughulika nayo, ghafla wananchi walipiga mayowe wakihoji babu Seya je, ndipo Lowassa aliamua kuahidi kuwaachia huru.
 
Awali awali akimkaribisha mgombea huyo, Menyekiti mwenza wa Ukawa, Freeman Mbowe, alitumia fursa hiyo kuonya juu ya mambo mawili kuelekea katika uchaguzi wa Oktoba 25 mwaka huu.
 
Mbowe alisema suala la uchakachuaji wa majina ya vijana katika daftari la wapiga kura ni hatari na kuomba Tume ya Taifa (NEC) kuepuka kufanya jambo hilo kwani litasababisha vurugu kubwa  kwa kuwa tayari kuna viashiria hivyo.
 
Pia alilitaka jeshi la polisi kuepuka na kuendeleza tabia ya kuwa wakala wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na badala yake kukaa upande wa pili wa historia kwa kuwa wananchi wanahitaji mabadiliko.
 
Makada wapya toka CCM
 
Mbowe alitumia mkutano huo kuwatambulisha makada wapya waliojiunga na chama hicho kutoka CCM ambao ni mbunge, Modestus Kiluf wa Mbarali, Mchungaji Luckson Mwanjale ambaye hata hivyo hakupanda jukwaani kukabidhiwa kadi, pamoja na Mwanasiasa mkongwe, Njelu Kasaka.
 
Kwa upande wake, Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ambaye alikuwa mwenyeji , aliwatuhumu viongozi wa CCM kuwa wameingiza shahada bandia za kupiga kura kwa lengo la kuchakachua kura Oktoba 25 Mwaka huu.
 
Alisema kuwa, kwa mujibu wa taarifa zilizoifikia Chadema ni kwamba kura shahada hizo za bandia ziliingizwa Mkoani Mbeya kutoka Mkoani Dodoma na  kwamba tayari  chama hicho kimeandaa mkakati wa kuhakikisha shahada hizo hazitumiki ili kuisaidia CCM kushindi.
 
Mbatia
 
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, akihutubia katika mkutano huo alisema  licha ya Rais Jakaya Kikwete kusema kuwa ni maadui wao wataendelea kuhubiri amani ili kujenga matumaini kwa wananchi ambao tayari wanahitaji mabadikiko.
"Tarehe 4 mwezi huu Rais Kikwete alituita wapinzani ni maadui, sisi tutaendelea kuhubiri amani, kuhubiri uungwana na watu wa Mbeya mmeweka historia na naomba wanambeya tusijaribu kuhubiri chuki " alisema Mbatia.
Alisema kuwa taifa linaviashiria vyote vya kugawanyika  ndio maana UKAWA wameamua kumsimamisha Lowassa  kugombea nafasi ya Urais jwa kuwa ndiye mtu pekee kwa sasa ndio anaweza kulirudisha taifa katika misingi yake ya umoja na amani.
 
Hali ilivyokuwa kabla na baada ya lowassa kuwasili Mbeya
 
Lowassa aliyewasili katika uwanja wa ndege majira ya saa 8:30 za mchana alilazimika kutumia muda wa saa mbili na nusu kutoka uwanjani wa ndege wa Songwe hadi eneo lililoandaliwa kwa ajili ya mkutano la Ruada Nzovwe umbali wa kilomita 30.
Hali hiyo ilisababisha askari polisi kufanya kazi ya ziada kumnasua kiongozi huyo kutoka katika makundi ya watu waliosimama barabarani kuzuia msafa wake kutoka uwanja hapo.
Ndani ya uwanja wa ndege wakati Lowassa anasubiriwa walijitokeza makada wa Chama cha Mapinduzi(CCM) ambao pia walikuwa wagombea ubunge na wabunge waliomaliza muda wao, Mchungaji Luckson Mwanjale aliyekuwa mkombea ubunge jimno la Mbeya vijijini na Dickson Kilufi wa Mbarali.

No comments