Header Ads

ad

Breaking News

Bafana Bafana yaiduwaza Hispania, yaichapa bao 1-0

Matthew Booth wa Afrika Kusini 'Bafana Bafana' akijaribu kumzuia mshambuliaji wa Hispania Fernando Torres (katikati), huku Tshepo Masilela akiwa makini kumsaidia katika mechi ya kimataifa ya kirafiki iliyopigwa kwenye Uwanja wa Free State mjini Bloemfontein,  Afrika Kusini. Afrika Kusini ilishinda bao 1-0.
 Afrika Kusini 'Bafana Bafana' imefanya mambo ya ajabu, baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Hispania, katika mchezo wa kirafiki uliochezwa nchini Afrika Kusini.

Bao pekee lililowapa raha Waafrika Kusini lilifungwa na Bernard Parker dakika ya 56, lililokamilisha furaha yao, hasa kwa kuwafunga mabingwa wa Kombe la Dunia na Ulaya, Hispania.

Katika mchezo mwingine wa kirafiki wa kimataifa uliozikutanisha timu za Ujerumani na England uliochezwa kwenye Uwanja wa Wembley ulimaliza kwa Three Lions kushindwa kulipa kisasi na kukubali kipigo cha bao 1-0.

England na Ujerumani walikutana kwa mara mwisho mwaka 2010 kwenye fainali za Kombe la Dunia na kukubali kipigo cha mabao 4-1 katika hatua ya robo fainali na kuyaaga mashindano hayo.


Bao pekee katika mchezo huo lilifungwa na beki wa Arsenal Per Martesacker katika ya 39 na kufanikiwa kudumu hadi mwisho wa mchezo huo.

No comments