Header Ads

ad

Breaking News

Micho aomba kazi Harambee Stars

Micho
KIGALI, Rwanda
KOCHA wa timu ya taifa ya Rwanda, Milutin Sredojevic ‘Micho’, anaitamani timu ya taifa ya Kenya ‘Harambee Stars’ kuifundisha.
Supersport.com limepata taarifa kwamba, Micho, Kocha wa Uganda ‘The Cranes’,  Bobby Williamson na kocha wa zamani wa Burundi, Adel Amrouche, ni miongoni mwa makocha wanaotajwa nchini Kenya.  
“Ninaweza kuthibtihsa kuwa, Micho, Amrouche na Williamson, wameeleza nia yao. Wametuma maombi ya kazi hiyo,” mtoa habari aliiambia supersport.com.
Kocha wa zamani wa El Mereikh, 'Micho' alihudhuria kwenye Uwanja wa Nyayao wakati Kenya ilipocheza na Burundi, katika mechi ya kuwania kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi ya ndani (CHAN),  kitu kilichotoa uvumi.
Pia, Amrouche yupo nchini Kenya, inawezekana kwa mazungumzo na Shirikisho la Soka Kenya.
Kenya hawana kocha mpaka sasa, baada ya Mfaransa Henri Michel, kuachia ngazi, baada ya kucheza mechi mbili za kirafiki na kuchapwa na timu za taifa za Afrika Kusini na Tanzania.
Awali, Kocha wa zamani wa Nigeria ‘Super Eagles’,  Samson Siasia, alikuwa akihusisha na kazi hiyo.
Harambee Stars itakwenda nchini Libya Jumamosi, ikiwa na wachezaji wake nyota wanaocheza nje, akiwemo Victor Wanyama, Arnold Origi, Ayub Timbe na Dennis Oliech.

No comments