Header Ads

ad

Breaking News

Mariga alamba fomu Parma kwa mkopo

Mariga
ROMA, Italia
KIUNGO wa timu ya Inter Milan ya Italia, MacDonald Mariga, amejiunga na klabu yake ya zamani ya Parma kwa mkopo mpaka mwishoni mwa msimu.
Kwa mujibu wa taarifa za mtu wa karibu na mchezaji huyo,  Mariga aliamua kukimbilia Parma ili aweze kupata nafasi ya kucheza mara kwa mara katika kikosi cha kwanza.
“Siwezi kuthibitisha kwamba, Mariga amejiunga Parma kwa mkopo.”
Taarifa zilizonukuliwa na vyombop vya habari vya Italia, vimesema mchezaji huyo alitoa sababu ya kuondoka mInter Milan.
"Ninakwenda Parma, pale ni nyumbani. Sikupata nafasi ya kucheza, sina nafasi,” alinukuliwa na mtandao wa Inter.
Reading FC waliripotiwa kutaka kumsajili miaka mitatu iliyopita, wakati akielekea kutua Manchester City.
Mariga ni mchezaji pekee kutoka Afrika Mashariki aliyefanikiwa kulibeba kombe la Ligi Kuu Italia ‘Serie A’ na Klabu Bingwa Ulaya.

No comments