Simba mwendo mdundo
![]() |
Juma Kaseja (kulia) na Mrisho Ngassa |
Hata hivyo, ushindi huo ulipatikana
huku timu hiyo ikiwa pungufu baada ya mshambuliaji wao Mganda Emmanuel Okwi
kutolewa kwa kadi nyekundu katika dakika ya 38, baada ya kumpiga kiwiko beki wa
JKT Ruvu, Kessy Mapande.
Pamoja na kumiliki vyema mpira
sehemu kubwa ya mchezo huo, JKT Ruvu walishindwa kabisa kuhimili vishindo vya
Simba inayodhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya
Kilimanjaro Lager, baada ya kujikuta ikilambwa mabao hao mawili.
Kwa ushindi huo wa pili mfululizo
kwenye uwanja wake wa nyumbani, Simba imefanikiwa kufikisha pointi sita na
hivyo kuwa kileleni kwenye msimamo wa ligi hiyo inayoshirikisha timu 14.
Kiungo mkabaji Amri Kiemba, ndiye aliyekuwa
wa kwanza kuipatia Simba bao katika dakika ya 47 baada ya shambulizi kali
ambapo mabeki wa JKT Ruvu walishindwa kuwa makini kuondosha hatari.
Katika dakika ya 72, Haruna Moshi
‘Boban’, aliipatia Simba bao la pili baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa
Mrisho Ngassa ambaye katika mchezo huo, alionekana kuwa mwiba mkali kwa JKT
Ruvu.
Bao hilo lilianzia kwa Ramadhani
Chombo ‘Redondo’ ambaye aliingia kuchuku nafasi ya Daniel Akuffo dakika ya 60
ambapo kiungo huyo aliwapangua walinzi wa JKT Ruvu na kutoa pasi kwa Ngassa.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo,
Kagera Sugar ilibanwa na Oljoro JKT kwenye uwanja wao wa nyumbani kwa suluhu,
huku Toto African ikipata sare ya mabao 2-2 na Azam Uwanja wa CCM Kirumba,
Mwanza, wakati Ruvu Shooting iliichapa Mgambo JKT mabao 2-1 kwenye Uwanja wa
Mkwakwani, Tanga.
Mjini Mbeya kwenye Uwanja wa
Sokoine, Prisons ya huko ilitoka sare ya bao 1-1 na Coastal Union ya
Tanga, wakati kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam, African Lyon iliichapa
Polisi Moro bao 1-0.
No comments