Header Ads

ad

Breaking News

Twite afufua 'sheshe' la Okwi


Emmanuel Okwi

Na Abdallah Mkwinda

KITENDO cha Yanga kufanikiwa kumnasa mchezaji wa FC Lupopo ya DRC anayekipiga kwa mkopo APR ya Rwanda, Mbuyi Twite, kimewashtua wapenzi wa Simba ambao wameanza kupata hofu juu ya majaliwa ya mshambuliaji wao, Emmanueli Okwi.

Awali, uongozi wa Simba ulijinadi kuwa ulishamalizana na Twite aliyeng’ara katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati iliyomalizika hivi karibuni jijini Dar es Salaam akiwa na APR, lakini juzi ziliibuka taarifa za Yanga kumnasa beki huyo kutokana na kazi nzuri iliyofanywa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo, Abdallah Bin Kleb.

Mwenyekiti wa Simba, Alhaji Ismail Aden Rage, aliwatangazia wanachama wa klabu yao katika mkutano uliofanyika wiki iliyopita kuwa Twite ni mali yao na kwamba alitarajiwa kutua jijini Dar es Salaam wakati wowote tayari kuitumikia klabu hiyo.

Lakini kitendo cha Wekundu wa Msimbazi hao kuzidiwa kete kwa mchezaji huyo kama SuperStar ilivyopasha juzi, wapenzi wa Simba sasa wamepatwa na mchecheto juu ya Okwi wakihofu kuporwa na watani wao hao wa jadi.

Okwi, ambaye aligonga kisiki katika majaribio nchini Australia, alirudi nchini kwao Uganda alikokaa kwa siku chache kabla ya kutua jijini Dar es Salaam kwa ajili ya tamasha la Simba, Simba Day lililofanyika Jumatano iliyopita kabla ya kurejea kwao Uganda siku iliyofuata.

Kosa walilofanya Simba Rwanda, linaweza kuendelekea tena Uganda ambapo baada ya mabingwa hao wa ligi  kushindwa kuweka mambo sawa, Yanga wamekwenda huku kwa lengo la kumalizana naye.

Hali hiyo ya Simba kushindwa kumalizana na Okwi,imepokelewa tofauti na mashabiki  na wanachama wa timu hiyo ,huku wakiutaka uongozi wafanye kila njia ili wahakikishe nyota huyo anabaki Msimbazi.

“Hakutakuwa na majadiliano kama Okwi akiondoka ,kwanini hawa viongozi wetu wanatufanyia hivi ,hii ni timu ya wanachama sio ya kwao ,”hiyo ni kauli ya mwanachama wa Simba.

Hatuwezi kuvumilia ,viongozi wamezidi kutuongopea ,kwanza walituambia Twite anakuja kumbe hakuna lolote na hili la Okwi ndio wanatupiga chenga,aliongeza mwanachama huyo ,ambapo alitoa kauli hiyo juzi usiku katika makao makuu ya Simba.

Wakati wa Simba ,ikishindwa kuongea na mchezaji huyo,viongozi wa Yanga wamelipokea suala hilo kwa furaha ambapo timu hiyo inamuhitaji mchezaji huyo kwa udi na uvumba.

Viongozi hao wa Yanga, ambao waliweza kufanya nae mazungumzo mchezaji huyo akiwa Uganda baada ya kurudi Australia ,sasa wameenda kumalizia picha hiyo ,ambapo mchezaji huyo yupo nchini kwao katika kikosi chake cha Taifa.

Habari ambazo Super Star ilizipata jana ni kwamba baada ya mchezaji huyo kumaliaza na Yanga ,atakuja nchini na mwanasheria wake ili aweze kuvunja mkataba wake na Simba.

Miongoni mwa sababu ambazo zinapelekea mchezaji huyo kusaka timu ya kuitumikia inatokana na viongozi wa Simba kushindwa kumtimizia mahitaji yake ikiwa ni pamoja na kumuongezea mshahara.

Mshambuliaji huyo ,ambaye aliliambia Super Star,kuwa amebakiza mwaka mmoja wa kuitumikia Simba  lakini  hayupo tayari kuongeza mkataba hadi pale watakapozungumza makubaliano mapya.

Katika mazungumzo hayo ,Okwi alikuwa anataka Dola za Marekani 80,000 kwa ajili ya kuongeza mkataba pamoja mshahara dola 3,000 kwa mwezi zikiwa ni kama milioni 4 za Tanzania.

Baada ya nyota huyo kutaka dau hilo viongozi wa Simba walionekana kutoafikiana na msimamo wa mchezaji huyo.

Kitendo cha kushindwa kupata majibu ya kuridhisha kwa nyota huyo wa Uganda juu ya ongezeko lake la mshahara kitaweza kuigharimu Simba katika msimu ujao.

Kama Yanga wakifanikiwa kupata saini ya mshambuliaji huyo watalazimika kumuacha mchezaji wao mmoja wa kigeni kwa mujibu wa kanuni za Shiriko la soka Tanzania(TFF).

Kanuni za TFF,linazitaka timu ambazo zinashiriki ligi kuu kuwa na wachezaji watano na sio vinginevyo.

Hadi sasa mabingwa hao wa Afrika Mashariki na Kati, wanawachezaji watano ambapo ni kipa Yaw Berko,Hamisi Kiiza,Haruna Niyonzima,Didie Kavumbago,pamoja na Mbuyu Twite na hivyo kama wakiipata saini ya Okwi atakuwa ni mchezi sita

No comments