Header Ads

ad

Breaking News

Simba watesa TBL Arusha

Na Mwandishi Wetu, Arusha

TIMU ya soka ya Simba, ambayo imeweka kambi mkoani Arusha, jana ilifanya ziara ya kutembelea kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kilichopo jijini Arusha. 

Akizungumza katika ziara hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi wa timu hiyo,  Ibrahimu Masoud ‘Maestro’, alisema kuwa, wao wameamua kufanya ziara katika kiwanda hicho, ili kujionea mambo mbalimbali yanayofanywa na kampuni hiyo inayozalisha bia ya Kilimanjaro Premium Lager, ambayo ndio wadhamini wakuu wa timu yao. 

Alisema kuwa, Kilimanjaro Premium Lager huwapa ushirikiano mkubwa katika mambo mbalimbali ya kimichezo, yakiwemo magari ya usafiri, jezi na vifaa mbalimbali vya michezo, hivyo wamefurahishwa mapokezi mazuri kiwandani hapo, na kuwaomba waendelee na moyo huo huo wa kuthamini timu yao.

Naye, Meneja wa bia ya Kilimanjaro, George Kavishe, kwa niaba ya TBL alisema kuwa, wamefurahishwa sana na ujio wa timu hiyo, kwa kuamua kuacha kazi zao na kutembelea kiwanda chao kuona jinsi wanavyofanya kazi. 

Alisema kuwa, TBL inathamini mchango wa timu za Simba na Yanga, kwa soka la Tanzania, na ndio maana imekuwa ikizidhamini timu hizo kwa muda mrefu, huku akibainisha kuwa, wataendelea kudhamini timu hizo hadi mwisho. 

Alisema kuwa, timu hizo hufanya mambo makubwa, kwani zimekuwa zikiwapatia vijana mbalimbali ajira, huku akiwasihi wananchi kuendelea kuziunga mkono timu hizo, kwani ndizo zenye wachezaji wengi wanaochezea timu ya taifa.

 Kavishe alisema kuwa, kupitia udhamini wa timu hizo, pia wamekuwa wakijitangaza sehemu mbalimbali, ikiwemo nje ya nchi, hivyo wanasaidia kuifanya kampuni na bia ya Kilimanjaro kuwa juu zaidi.


 Wachezaji na viongozi wa klabu ya Simba wakitembelea kiwanda cha TBL kilichopo Arusha mwishoni mwa wiki ili kujionea uzalishaji wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambayo ndio mdhamini wao mkuu
 Kocha Mkuu wa Simba, Profesa Milovan Cirkovic akiongea na Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe kwenye hafla iliyofanyika baada ya wachezaji na viongozi wa klabu ya Simba kutembelea kiwanda cha TBL kilichopo Arusha mwishoni mwa wiki ili kujionea uzalishaji wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambayo ndio mdhamini wao mkuu.
 Mratibu wa Usalama na Afya wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Kassena Heavy, akiwaeleza jambo wachezaji na viongozi wa klabu ya Simba waliotembelea kiwanda cha TBL kilichopo Arusha mwishoni mwa wiki ili kujionea uzalishaji wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambayo ndio mdhamini wao mkuu.
 Wechezaji wa klabu ya Simba wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kilichopo Arusha mwishoni mwa wiki ili kujionea uzalishaji wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambayo ndio mdhamini wao mkuu
Mratibu wa Usalama na Afya wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Kassena Heavy, akiwaeleza jambo wachezaji na viongozi wa klabu ya Simba waliotembelea kiwanda cha TBL kilichopo Arusha mwishoni mwa wiki ili kujionea uzalishaji wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambayo ndio mdhamini wao mkuu
Kocha Mkuu wa Simba, Profesa Milovan Cirkovic akitoa neon la shukrani baada ya wachezaji na viongozi wa klabu ya Simba kutembelea kiwanda cha TBL kilichopo Arusha mwishoni mwa wiki ili kujionea uzalishaji wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambayo ndio mdhamini wao mkuu. Kulia kwake ni Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe na Meneja wa Vifaa wa Klabu ya Simba, Kessy Hassan. Picha: Executive Solutions

No comments