Header Ads

ad

Breaking News

Miss East Africa kuoneshwa ‘live’ na MNET


Mwakilishi wa Seychelles katika mashindano ya Miss East Africa- Annabelle Marvel Pointe (19)

Na Mwandishi Wetu
MASHINDANO ya urembo ya Afrika Mashariki yamepangwa kuoneshwa moja kwa moja kupitia Mnet, ambapo yatashuhudiwa na  watu wanaokadiliwa kufikia  milion 200, kupitia televison na kwa njia ya internet duniani kote.

Awali, mashindano hayo yanayozishirkisha nchi za Kenya, Uganda, Ethiopia, Sudan Kusini, Tanzania, Kenya, Rwanda, Burundi, Comoro, Shelisheli na nyingine, yalipangwa kufanyika Septemba mwaka huu, lakini yamesogezwa mbele hadi Desemba 7.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Kampuni ya Rena Events Ltd ya jijini Dar es Salaam, Rena Callist ambao ndio waandaaji wa mashindano hayo, alisema kuwa, mashindano hayo yatafanyika katika ukumbi wa Mlimani City  jijini Dare s Salaam.

Alisema uamuzi wa kusogeza mbele tarehe ya mashindamo hayo, ni kutoa nafasi kwa nchi ambazo hazijapata wawakilishi wao katika mashindano hayo.

Mashindano ya Miss East Africa mwaka huu yanatarajiwa kuwa na mvuto wa aina yake, ambapo yatashirikisha warembo kutoka katika nchi 16 za ukanda wa Afrika Mashariki.

Nchi zilizothibitisha kushiriki mashindano hayo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi, wakati zilizoalikwa ni Ethiopia, Eritrea, Somalia, Djibouti, Sudan Kusini, Malawi, visiwa vya Shelisheli, Madagascar, Reunion, Comoros na Mauritius.

Alisema mashindano ya Miss East Africa yanalenga kukuza ushirikiano na kutangaza utamaduni wa Afrika Mashariki, utalii wa Tanzania kama nchi mwenyeji wa mashindano hayo makubwa katika ukanda huu wa Afrika 

Baadhi ya nchi zitakazoshiriki mashindano hayo ambazo zimewatangaza wawakilishi wao ni Eritrea, Ethiopia, Uganda, Sudan Kusini, Malawi na Shelisheli. 

Callist alisema nchi zinatarajia kutangaza wawakilishi wao kabla ya tarehe ya mwisho ambayo ni Septemba 28,  mwaka huu.

Miss East Africa Uganda-Ayisha Nagudi (23)

Miss East Africa Ethiopia-Lula Teklehaimanot (19

Miss East Africa Eritrea-Rahwa Afeworki (22)

No comments