WASWAZI KUCHEZESHA SIMBA, AL AHLY SHANDY
![]() |
Simba |
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka Swaziland
kuchezesha mechi ya kwanza ya 16 bora ya Kombe la Shirikisho kati ya
Simba na Al Ahly Shandy ya Sudan itakayochezwa Aprili 29 mwaka huu
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Waamuzi
hao wa mechi hiyo namba 71 ni Nhleko Simanga Pritchard atakayepuliza
filimbi wakati wasaidizi wake ni Mbingo Petros Mzikayifani na Sibandze
Thulani. Mwamuzi wa mezani atakuwa Fakudze Mbongiseni Elliot.
CAF pia imemteua Kayijuga Gaspard wa Rwanda kuwa Kamishna wa mechi hiyo.
No comments