KAMPUNI NNE ZAPITA TENDA YA TIKETI
![]() |
Wambura |
Kampuni
nne kati ya sita zimepita hatua ya kwanza ya mchakato wa kupata moja
itakayofanya kazi ya kutengeneza tiketi za elektroniki kwa ajili ya
mechi za Ligi Kuu ya Vodacom na nyingine zinazosimamiwa na Shirikisho la
Kimataifa la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Shughuli
ya ufunguzi wa maombi ya hatua ya awali ya kuonesha nia (Expression of
Interest) kwa ajili ya tenda hiyo ilifanywa jana (Aprili 19 mwaka huu)
na Kamati ya Mipango na Fedha ya TFF ambayo ndiyo Bodi ya Tenda ya
shirikisho.
Kampuni
ambazo zimepita hatua hiyo ya kwanza sasa zinatakiwa kuwasilisha rasmi
tenda zao kwa ajili ya shughuli hiyo ndani ya kipindi cha wiki tatu
tangu ulipofanyika ufunguzi wa hatua ya kwanza.
Baadaye
Bodi ya Tenda itakutana tena kupitia tenda zitakazokuwa zimewasilishwa
na kufanya uteuzi wa kampuni moja itakayofanya kazi hiyo.
Kampuni
ambazo zimefanikiwa kuingia katika hatua hiyo ya pili ni CRDB Bank PLC,
SKIDATA People Access Inc., Prime Time Promotions na Punchlines (T)
Limited.
No comments