Ligi Kuu kutimka kesho viwanja viwili
Ligi
Kuu ya Vodacom inaingia raundi ya 24 wikiendi hii kwa mechi mbili
zitakazochezwa Aprili 22 jijini Dar es Salaam. Villa Squad itaumana na
African Lyon kwenye Uwanja wa Chamazi wakati Yanga itakuwa mwenyeji wa
Polisi Dodoma katika Uwanja wa Taifa.
Azam
na Mtibwa Sugar zilizokuwa zicheze Aprili 21 mwaka huu sasa zitacheza
Aprili 23 mwaka huu kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam wakati siku
hiyo hiyo jioni kutakuwa na mechi kati ya Simba na Moro United. Mechi
zote zitaanza saa 10.30 jioni.
Aprili
25 mwaka huu Oljoro JKT itaikaribisha Yanga kwenye Uwanja wa Kumbukumbu
ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha wakati JKT Ruvu itakuwa
mwenyeji wa Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.
Raundi
ya 25 itakamilika kwa mechi nne; Aprili 28 mwaka huu Coastal Union
itakuwa mwenyeji wa Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga
huku Mtibwa Sugar ikiwa mgeni wa African Lyon kwenye Uwanja wa Chamazi.
Azam na Toto African zitacheza Chamazi, Aprili 30 mwaka huu wakati Mei 1
mwaka huu Villa Squad itaumana na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Chamazi.
Ligi
hiyo itafunga msimu wa 2011/2012, Mei 5 mwaka huu ambapo timu zote 14
zitakuwa uwanjani. Simba vs Yanga (Uwanja wa Taifa), Oljoro JKT vs
Polisi Dodoma (Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha), Ruvu Shooting vs Villa
Squad (Mabatini, Mlandizi), Coastal Union vs Toto African (Mkwakwani,
Tanga), African Lyon vs JKT Ruvu (Manungu, Morogoro), Azam vs Kagera
Sugar (Chamazi, Dar es Salaam) na Moro United vs Mtibwa Sugar (Jamhuri,
Morogoro).
No comments