Poulsen aahidi ushindi Ngorongoro Heroes leo
![]() |
Poulsen |
Kocha
Kim Poulsen anayeinoa timu ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 cha
Tanzania (Ngorongoro Heroes) ameahidi kikosi chake kufanya vizuri kwenye
mechi dhidi ya Sudan.
Akizungumza
jana (Aprili 20 mwaka huu) kwenye mkutano na Waandishi wa Habari,
Poulsen amesema timu yake imejiandaa vizuri kwa mechi hiyo na kiu yao ni
kushinda.
Kwa
upande wake Kocha wa Sudan, Azhari Osman El Tahir amesema ingawa
haifahamu vizuri timu ya Tanzania, lakini wamejiandaa kushinda kwani kwa
muda mrefu walikuwa hawajashiriki mashindano ya vijana ya kimataifa.
Mechi
hiyo ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri huo itachezwa kesho
(Aprili 21 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10
kamili jioni kwa viingilio vya sh. 3,000, sh. 5,000, sh. 10,000 na sh.
15,000.
Sudan
iliwasili nchini jana (Aprili 19 mwaka huu) ikiwa na kikosi cha
wachezaji 20, viongozi kumi na mwandishi wa habari mmoja kwa ajili ya
mechi hiyo ya kwanza kabla ya timu hizo kurudiana jijini Khartoum kati
ya Mei 4, 5 na 6 mwaka huu.
Mechi
hiyo itachezeshwa na mwamuzi Brian Miiro atakayesaidiwa na Mark Ssonko,
Lee Patabali na Denis Batte wote kutoka Uganda. Ejigu Ashenafi wa
Ethiopia ndiye atakayekuwa Kamishna wa mechi hiyo namba 15.
Fainali
za Afrika kwa michuano hiyo zitafanyika Machi mwakani nchini Algeria
wakati za Dunia zitafanyika nchini Uturuki kuanzia Juni hadi Julai
mwakani. Katika fainali za Dunia, Afrika itawakilishwa na timu nne za
kwanza kwenye fainali za Algeria.
No comments