MALINZI MGENI RASMI MKUTANO MKUU TFF LEO
![]() |
Dioniz Malinzi |
Mwenyekiti
wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Dioniz Malinzi anatarajia kuwa
mgeni rasmi kwenye ufunguzi Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Shirikisho la Mpira
wa Miguu Tanzania (TFF) utakaofanyika kwa siku mbili (Aprili 21 na 22
mwaka huu) kwenye ukumbi wa NSSF Waterfront jijini Dar es Salaam.
Wajumbe
wa mkutano huo watawasili jijini kesho (Aprili 20 mwaka huu) na
watafikia kwenye hoteli ya Royal Valentino. Wajumbe wanatoka katika
vyama vya mpira wa miguu vya mikoa, vyama shiriki na klabu za Ligi Kuu
ya Vodacom.
Mkutano
huo utakaoanza saa 3 asubuhi utakuwa na ajenda kumi na moja. Baadhi ya
ajenda hizo ni hotuba ya Rais wa TFF, taarifa ya utendaji ya mwaka 2011,
bajeti ya mwaka 2012 na taarifa ya ukaguzi wa hesabu (audited
accounts).
No comments