Header Ads

ad

Breaking News

Simba gonjwa lile lile

Simba wakiwasalimia wachezaji wa URA, kabla ya kuanza kwa mechi, leo.


 *Yatandikwa mabao 2-0 na URA

MABINGWA wa soka Tanzania Bara, Simba, jana walianza vibaya michuano ya Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame), baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0, dhidi ya Kodi ya Mapato Uganda (URA), katika mechi iliyopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Katika mchezo huo, ambao ulianza kwa kila timu kulisakama lango la wenzake, dakika ya nane, Mwinyi Kazimoto wa Simba alipata nafasi nzuri, lakini shuti lake kali lilitoka nje ya lango la wapinzani wao.

Ali Feni wa URA, aliipatia timu yake bao la kwanza dakika ya 11, kwa kichwa baada ya kuunganisha mpira uliitoka kwa Owen Kasule, akimwacha kipa wa Simba Juma Kasema akiruka bila mafanikio.

Wakicheza kwa kujiamini, URA ilipata nafasi nyingine nzuri dakika ya 13, wakati Robert Ssentogo alipomjaribu Kaseja kwa shuti kali lililopita karibu na lango la Simba.

Danny Mrwanda alishindwa kutumia vizuri pasi iliyotoka kwa Mussa Mudde, baada ya kubaki na kipa wa URA, Yassin Mugabi na kupiga shuti lililotoka nje ya lango.

Simba walizidisha mashambulizi, ambapo dakika ya 38, Mudde alimjaribu kwa shuti la mbali kipa wa URA, Mugabi, ambaye alilipangua, lakini Mrwanda alichelewa kuufuata mpira na kumpa nafasi kipa huyo kuudaka.

Dakika ya 55, Felix Sunzu wa Simba, alipata nafasi nzuri, lakini alishindwa kuunganisha mpira wa krosi uliopigwa na Abdallah Juma aliyeingia kuchukua nafasi ya Mrwanda.

Simba wakijitahidi kuongeza mashambulizi ya kusaka bao la kusawazisha, walijikuta wakichapwa bao la pili dakika ya 88, lililofungwa na Ali Feni kwa kichwa akiunganisha mpira uliopigwa na Simeon Masaba aliyemtoka Amir Maftah na kumpasia mfungaji wa bao hilo.
Kipigo hicho ni sawa na kile walichokipata watani wao wa jadi Yanga, baada ya kuchapwa na Atletico ya Burundi mabao 2-0. Hivyo, vigogo hao hakuna wa kumcheka mwenzake.


Simba: Juma Kaseja, Haruna Shamte, Amir Maftah, Obadia Mungusa, Juma Nyoso,Mussa Mudde, Felix Sunzu, Amri Kiemba/Uhuru Seleman, Mwinyi Kazimoto, Danny Mrwanda/Abdalla Juma, Kanu Mbiyavanga/Haruna Moshi ‘Boban.

URA: Yassin Mugabi, Simeon Massa, Alan Munaaba, Derrick Walulya, Samuel Ssenkoomi, Oscar Agaba, Ali Feni, Owen Kasule/Augustine Nsumba, Ssentongo, Said Kyeyune/ Sula Bagala, Yayo Lutimba/Farouk Wejuli.

Kutoka Uwanja wa Azam Chamazi, wamiliki wa uwanja huo, Azam FC, jana ilishindwa kuutumia vizuri uwanja wake, baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Mafunzo ya Zanzibar.
Katika kundi, URA inaongozwa ikifuatiwa na Azam na Mafunzo, huku Simba ikiwa ya mwisho.

cio

No comments