Header Ads

ad

Breaking News

Morogoro Bingwa Copa Coca Cola 2012


TIMU ya soka ya Mkoa wa Morogoro jana ilitwaa ubingwa wa Copa Coca Cola, baada ya kuilaza Mwanza bao 1-0, katika mchezo wa fainali uliopigwa kwenye Uwanja wa Kambukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam, leo.

Washindi walipata bao pekee kipindi cha kwanza lililofungwa na Salum Ramadhan kwa shuti kali lililokwenda moja kwa moja wavuni.

Katika mchezo huo, timu zote zilikuwa zikishambuliana kwa zamu, lakini makipa wa timu zote mbili walikuwa makini kuhakikisha nyavu zao hazitikiswi.

Bingwa mpya wa michuano hiyo alizawadiwa Morogoro amekabidhiwa kombe na hundi y ash. milioni nane, wakati mshindi wa pili Mwanza wakizawadiwa sh. milioni 4.8.

Temeke ambao walishinda nafasi ya tatu walipewa sh. milioni 3.2, zawadi zote hizo zimetoka kwa waandaaji wa mashindano hayo kampuni ya Coca Coca Cola nchini.

Mara baada ya mchezo huo kumalizika, Kocha wa Morogoro, Mecky Mexime, alisema kuwa, hakutegemea vijana wake kama wangeweza kuibuka na ushindi katika mchezo huo.

“Mchezo ulikuwa mkali na mgumu, sikutegemea kama vijana wangu wangeweza kuibuka na ushindi, nashukuru wametimiza ndoto zetu,” alisema.

No comments