Header Ads

ad

Breaking News

Rwanda U20 yawasili kuikabili Ngorongoro Heroes


Ngorongoro Heroes
TIMU ya taifa ya Rwanda ya vijana wenye umri chini ya miaka 20, imewasili jijini Dar es Salaam jana, kwa ndege ya RwandAir kwa ajili ya mechi mbili za kirafiki dhidi ya Ngorongoro Heroes.
 
Rwanda yenye msafara wa watu 27 wakiwemo wachezaji 20, itafikia hoteli ya Sapphire, ambapo mechi hizo zitachezwa leo kwenye Uwanja wa Chamazi na Julai 16, mwaka huu Uwanja wa Taifa.
 
Ngorongoro Heroes tayari iko kambini chini ya Kocha Jakob Michelsen na msaidizi wake Adolf Rishard, kujiwinda kwa mechi hizo ambazo ni sehemu ya maandalizi ya kuivaa Nigeria.
 
Mechi dhidi ya Nigeria ambayo ni ya kwanza ya raundi ya pili kusaka tiketi ya kucheza fainali za Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Algeria itachezwa Julai 29 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

No comments