Header Ads

ad

Breaking News

Mwanza kucheza fainali Copa Coca Cola Jumapili


TIMU ya Mkoa wa Mwanza imekata tiketi ya kucheza fainali ya michuano ya Copa Coca-Cola 2012 iyakayopigwa Jumapili, baada ya leo asubuhi kuilaza Temeke mabao 3-1, katika mchezo wa nusu fainali uliofanyika Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam.
 
Hadi dakika 90 zinamalizika, timu hizo zilikuwa zimefungana bao 1-1.
Mwanza walipata bao lao dakika ya tatu kupitia kwa Jamal Mtegeta, kabla ya Temeke kusawazisha kwa penalti dakika ya 56, iliyowekwa wavuni na Baraka Ntalukundo.
 
Mabao mengine ya Mwanza yaliyoipatia tiketi ya kucheza fainali kesho yalifunga dakika 30 za nyongeza, kupitia kwa Mtegeta dakika ya 94, kabla ya Dickson Ambundo kukwamisha la tatu dakika ya 108.
 

No comments