Header Ads

ad

Breaking News

KIMANJARO PREMIUM LAGER YAKABIDHI SIMBA NA YANGA VIFAA VYA KOMBE LA KAGAME


Kaimu Meneja wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Oscar Shelukindo (kulia), akimkabidhi Meneja wa Yanga, Hafidh Suleiman, vifaa kwa ajili ya mashindano ya Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame), yanayoanza leo. Makabidhiano hayo yalifanyika jijini Dar es Salaam, jana. (Picha: Executive Solutions)

Ikiwa ni sehemu ya udhamini wake, Kilimanjaro Premium Lager imezikabidhi timu za Simba na Yanga vifaa kwa ajili ya michuano ya Kombed la Kagame iliyopangwa kuanza wikendi hii jijini Dar es salaam. Kaimu Meneja wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Oscar Shelukindo alisema: “Bila shaka Simba na Yanga ni klabu kubwa zaidi nchini Tanzania na zote kwa pamoja zimefika fainali za Kombe la Kagame mara 18, jambo ambalo ni mafanikio makubwa sana kwa timu hizi. Kama mdhamini mkuu wa timu hizi, Kilimanjaro Premium Lager imeona umuhimu wa kuziunga mkono klabu hizi katika jitihada zake kutuletea tena fainali yenye burudani.” Alisema.

Aliongeza kuwa Kombe la Kagame ndio mashindano makubwa zaidi ya yanayohusisha vilabu katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na ni fursa zuri kwa wachezaji wetu kuonyesha vipaji vyao kwa kushindana na wachezaji bora zaidi wa soka katika ukanda huu na pia ni fursa nyingine kwa wanaohusika na timu ya taifa kuweza kuchagua wachezaji.

 “Ushirikiano kati ya Kilimanjaro Premium Lager na klabu hizi umejikita katika mambo yanayotuunganisha kama vile ushirikiano, umoja na kujituma kufanya kilicho bora. Tunaendelea kutimiza wajibu wetu kwa klabu hizi na tuko tayari kupeleka mpira wa Tanzania kwenye kilele cha mafanikio.” 

Kaimu Meneja huyo pia aliwasihi Simba na Yanga kuhakikisha wanaiwakilisha nchi vizuri katika mashindano haya makubwa kikanda na kuwafanya Watanzania wajivunie klabu hizo kwa kuiletea Tanzania ushindi wa kombe la Kagame kwa mara ya 11.
Kaimu Meneja wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Oscar Shelukindo (kushoto), akimkabidhi Makamu Mwenyekiti wa Simba, Godfrey Nyange, vifaa kwa ajili ya mashindano ya Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame), yanayoanza leo. Makabidhiano hayo yalifanyika jijini Dar es Salaam, jana.  (Picha: Executive Solutions)

No comments