Header Ads

ad

Breaking News

TFF YATAKA WALIOVURUNDA KUPANGA RATIBA YA LIGI KUU BARA 2017-18 WACHUKULIWE HATUA

Kaimu Katibu Mkuu TFF, Kidao Wilfred (katikati), Salum Madadi (kulia) na Alfred Lucas, Msemaji wa shirikisho hilo.
Na.Alex Sonna
Shirikisho la Mpira wa Miguu  nchini TFF chini ya Rais Mpya Wales Karia,limepanga kuwachukulia hatua ya kinidhamu viongozi wa bodi ya Ligi wote ambao walihusika na upangaji wa ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara msimu wa mwaka 2017-18 wakiongozwa na Bonifance Wambura ambaye ndio mhusika Mkuu katika swala la ratiba.

Akizungumza na waandishi wa habari Kaimu Katibu Mkuu wa TFF,Wilfred Kidao amesema kuwa uongozi wa shirikisho hilo umeamua kuchukua jukumu hilo baada ya kubaini wataalamu hao wameshindwa kupanga vizuri ratiba ya ligi hivyo Rais wa TFF,Wallace Karia ametoa agizo kwa mtendaji wa bodi ya ligi achukue Jukumu la kuwachukulia hatua wale wote waliohusika na hatua hiyo.
“Nimeagizwa na rais nimwandikie barua mtendaji mkuu wa bodi ya ligi ili aweze kuwachukulia hatua viongozi wa bodi hiyo waliohusika na kupanga ratiba hii pamoja na kwamba walikuwa na kalenda lakini bado wamekosea,” alisema Kidao.
Kidao amesema kuwa ratiba hiyo ilipangwa kwa makosa makubwa hivyo kupelekea kuwa na dosari mapema baada ya kuchezwa mechi moja tu ya Ligi Tayari imeanza kupanguliwa kutokana na kuingiliana na Kalenda ya FIFA hivyo kusababisha Ligi Kuu Kusimama kwa muda kupisha mechi ya Kirafiki kati ya Tanzania na Botswana inayotarajiwa kuchezwa siku ya Jumapili kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.
Aidha amesema kuwa TFF  imetoa agizo kwa uongozi wa bodi ya ligi kuiangalia upya ratiba hiyo ya ligi na pia imeteua kikosi cha watu wa nne ambacho kitakuwa na jukumu la kuifanyia marekebisho ya msingi ratiba hiyo ambayo hayataleta athari katika ligi hiyo.
Kwa kumalizia Kidao amesema kuwa kamati aliyeiteua inatakiwa kufika mpaka siku ya Jumapili iwe imeshampelekea ratiba yote na kwa sasa Bodi ya Ligi haitaweza kutoa ratiba ya Ligi bila kupitiwa na Katibu Mkuu wa TFF hivyo Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi ni Boniface Wambura ambaye sasa atakuwa na jukumu la kuchukua hatua kwa wasaidizi wake.

No comments