MAJINA NANE YAPITISHWA MCHUJO WA AWALI UONGOZI TPLB
Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la
Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imetangaza majina manane ya wagombea ambao
yamepita katika mchujo wa awali kuwania nafasi mbalimbali katika Kamati ya
Uongozi (Management Committee) ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara.
Waliopitishwa kuwania uenyekiti wa
Management Committee ni Clement Sanga na Ahmed Yahya wakati Shan Crysostoms amepitishwa
kuwania nafasi ya makamu mwenyekiti.
Kwa mujibu wa kamati hiyo, Ramadhan
Mahano na Hamisi Madaki wamepitishwa kuwania nafasi ya Ujumbe wakitokea klabu
za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
James Bwire na Almas Kasongo
wamepitishwa kuwania ujumbe wakitokea klabu za Ligi Daraja la Kwanza. Brown
Ernest hakupitishwa kwa sababu hakuthibitishwa na klabu yake.
Edga Chibura amepitishwa kuwania
ujumbe akitokea klabu za Ligi Ligi Daraja la Pili.
Wagombea kwa mujibu wa kanuni za
uendeshaji wa Bodi ya Ligi Kuu ni marais au wenyeviti wa klabu husika. Wagombea
wanatakiwa kuwa wenyeviti au marais wa klabu husika.
Nafasi ya Mwenyekiti na Makamu
Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania inagombewa na klabu za Ligi Kuu pekee.
Wachezaji wote kutoka klabu za
Tanzania wamefika kadhalika baadhi kutoka nje ya mipaka ya Tanzania kama vile
Nahodha Mbwana Samatta na Elias Maguli. Mazoezi hayo yataendelea kila siku hadi
Ijumaa wiki hii.
Kikosi hicho kinachofanya mazoezi
chini ya Kocha Mkuu, Salum Shabani Mayanga kinajindaa kucheza na Botswana
katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa chini ya utaratibu wa kalenda ya Shirikisho
la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).
Wiki ya FIFA kwa mechi za kimataifa
inatarajiwa kuanza Jumatatu Agosti 28 hadi Septemba 5, mwaka huu ambako
Tanzania imekubaliana kucheza Botswana kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es
Salaam Jumamosi ya Septemba 2, 2017.
Katika kikosi hicho cha wachezaji
21, Kocha Mayanga amemwita upya Mlinzi wa Young Africans, Kelvin Yondani huku
nyota kutoka nje ya mipaka ya Tanzania wakiwa ni saba.
Kikosi hicho kinachopiga kambi
hoteli ya Sea Scape iliyoko Kunduchi, Dar es Salaam kina makipa Aishi Manula
(Simba SC), Mwadini Ally (Azam FC) na Ramadhani Kabwili (Young Africans).
Walinzi ni Gadiel Michael (Young
Africans), Boniphas Maganga (Mbao FC), Abdi Banda (Baroka FC/Afrika Kusini),
Kelvin Yondani (Young Africans), Salim Mbonde (Simba SC) na Erasto Nyoni (Simba
SC).
Viungo ni Himid Mao - Nahodha
Msaidizi (Azam FC), Hamis Abdallah (Sony Sugar/Kenya), Mzamiru Yassin (Simba
SC), Said Ndemla (Simba SC), Saimon Msuva (Difaa El Jadidah/Morocco), Shiza
Kichuya (Simba SC), Farid Mussa (CD Tenerif/Hispania) na Orgenes Mollel (FC
Famalicao/Ureno).
Washambuliaji ni Raphael Daud (Young
Africans), Kelvin Sabato (Azam FC), Mbwana Samatta (KRC Genk/Ubelgiji) na Elias
Maguli (Dhofar FC/Oman).
Benchi la Ufundi la Mayanga
linaundwa na yeye mwenyewe ambaye ni Kocha Mkuu, Fulgence Novatus (Kocha
Msaidizi), Patrick Mwangata (Kocha wa Makipa), Danny Msangi (Meneja), Dkt.
Richard Yomba (Daktari wa timu), Dkt. Gilbert Kigadye (Daktari wa Viungo) na
Ally Ruvu (Mtunza Vifaa).
Uchaguzi huo wa kamati hiyo
utafanyika Jumapili Oktoba 15, 2017 jijini Dar es Salaam na unaendeshwa kwa
mujibu wa kanuni za Uchaguzi za TFF toleo la 2013.
Katika hatua nyingine, Shirikisho la
Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetoa Ngao ya Jamii mpya kwa ajili ya kuipa
Simba ambayo ilifanikiwa kuishinda Young Africans katika mchezo kuwania taji
hilo uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Agosti 23, mwka huu.
-4, TFF ilitoa Ngao ya Jamii ambayo
ilikuwa na makosa ya maandishi yaliyoonekana kwenye hivyo kuzua taharuki kwa
wanafamilia wa mpira wa miguu.
No comments