Header Ads

ad

Breaking News

Conor McGregor kumfikia utajiri Cristiano Ronaldo

Conor McGregor alipokutana na Cristiano Ronaldo
DUBLIN,  Ireland
 Conor McGregor amejipa matumaini ya kumpita kwa utajiri nyota wa Ureno na klabu ya Real Madrid ya Hispania, Cristiano Ronaldo katika jaridi la Forbes kufuatilia pambano lake dhidi ya Floyd Mayweather.


Bondia huyo kutoka Dublin, pamoja na kuchapwa kwa Ko dhidi ya Mayweather anatarajia kuingiza Zaidi ya dola milioni 77, kabla ya mkataba wake.

Ronaldo anaongoza kwa utajiri kwa mwaka huu akiingiza Zaidi ya dola milioni 71, wakati McGregor juzi alipigwa kwa Ko katika raundi ya 10 na bingwa wa masumbwi duniani Mayweather, katika pambano lililofanyika Las Vegas.

Conor McGregor alikutana na Cristiano Ronaldo mwaka jana na kumwambia anataka kumpita kimpata katika listi ya utajiri.

McGregor atakuwa nyuma ya Floyd Mayweather, wakati Forbes watakapotioa viwango vipya.

Ronaldo alimtembelea bingwa huo UFC katika kambi yake ya mazoezi na bondia huyo alimweleza: 'Upo katika nafasi ya kwanza katika listi ya matajiri kwenye jarida la Forbes, nilikuwa namba 35 au namba Fulani hivi. Nitapanda. Inawezekana mwaka ujao nitakufikia.' Ronaldo alimjibu: 'Sidhani kama utafika niliko.'

No comments