Header Ads

ad

Breaking News

Waziri Profesa Ndalichako afanya ziara mkoani Iringa

IMG_1466
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Joyce Ndalichako   akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Richard Kasesela kushoto ni Mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa.

 
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Joyce Ndalichako  amefanya ziara katika shule za mkoani Iring zinazofundisha watoto wenye mahitaji maalumu ikiwemo ya Makala wilayani Mfundi, Viziwi Mtwivila, Sekondari ya Wasichana Mtwivila na Sekondari ya Lugalo. 
Leongo la ziara yake ni kukagua vifaa vya kufundishia vinavyotolewa na Serikali.
Joyce alipata fursa ya kusalimia wanafunzi na walimu za shule hizo, ambapo aliongzana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa,  Amina Masenza, Katibu Tawala wa mkoa huo, Wamoja Ayoub, Wakuu wa wilaya ya Mufindi, Jamhuri David na Iringa Mjini, Richard Kasesela.
Wengine walioambatana naye katika ziara hiyo ni  mbunge wa Viti Maalumu mkoani humo, Ritta Kabati, Zainab Mwamwindi na Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa.

IMG_1481
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Joyce Ndalichako  kizungumza  pamoja na viongozi mbalimbali mkoani Iringa wakifurahia jambo na wanafunzi wa shule ya maalum ya viziwi mkoani humo
IMG_1647
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Joyce Ndalichako akisalimiana na Mbunge wa Iringa mjini, Mchungaji Peter Msigwa  katika Shule ya Viziwi, kulia ni Mbunge Viti Maalumu, Zainab Mwamwindi na Mbunge wa Viti Maalumu Iringa, Ritha Kabati, wakiwaaangalia.
IMG_1855
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Joyce Ndalichako akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi nawalimu wakati wa ziara yake mkoani Iringa.
IMG_1867
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Joyce Ndalichako akiwa na wanafunzi wa Sekobdari ya Wasichana Iringa.
IMG_1940
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Joyve Ndalichako akizungumza na wananfunzi wa kidato cha tano wa Shule ya Sekondari Lugalo.

No comments