MATUKIO MBALIMBALI KUTOKA MOSHI KWENYE MSIBA WA NDESAMBURO,VIONGOZI WA CHADEMA WAKIPOKEA MWILI WA MAREHEMU
MWENYEKITI wa Chadema, Freeman Mbowe na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa wameupokea
mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema, Kilimanjaro, Phillemon
Ndesamburo katika viwanja vya Majengo mkoani hapa.
Ndesamburo alifariki wiki iliyopita wakati akipata matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC.
Mwili wa Ndesamburo aliyeliongoza Jimbo la Moshi Mjini kwa miaka 15, akiwa Mbunge,unaagwa katika viwanja hivyo na saa 10 jioni ulipelekwa
nyumbani kwake kwa ajili ya taratibu za mazishi.
Wabunge na viongozi wa Chadema, akiwamo muasisi wa chama
hicho, Edwin Mtei, Frederick Sumaye wapo uwanjani hapo kwa ajili ya
kumuaga Ndesamburo, wakiungana na mamia ya wafuasi na wakazi wa mikoa ya Kaskazini.

Matukio mbalimbali kutoka Moshi mkoani Kilimanjaro kwenye msiba wa
Marehemu Mzee Philemon Ndesamburo aliyefariki hivi karibuni mkoani humo,
Marehemu Ndesamburo aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa
Kilimanjaro na Mbunge wa jimbo la Moshi mjini utaagwa kwenye uwanja wa
Majengo kuanzia leo na kesho na kisha kuzikwa mkoani humo haya ni
matukio kadhaa ya picha za matukio yanayoendelea katika msiba huo.

Baadhi ya wa vijana waendesha bodaboda wakijiandaa kwa ajili ya
maandamano maalum wakati mwili wa marehemu utakapokuwa akipelekwa kwenye
uwanja wa Majengo.

Gari Maalum litakalochukua mwili wake.

Eneo la Uwanja wa Majengo ambalo ndipo shughuli za kuaga mwili zitafanyika likiwa limepambwa tayari kwa shughuli hizo. CLEO24NEWS
No comments