Header Ads

ad

Breaking News

Dennis Rodman, Mmarekani rafiki wa Kim Jong-un arudi tena Korea Kaskazini

North Korean leader Kim Jong-Un and Dennis Rodman watching a basketball game in Pyongyang in 2013
Rais wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un (kushoto) akiwa na 'rafiki yake wa maisha', Dennis Rodman (kulia) ambaye ni mcheza kikapu wa zamani wa Marekani.
 
BEIJING, China
MCHEZAJI wa zamani wa mpira wa kikapu, Dennis Rodman amerejea Korea Kaskazini katika kile kinachoelezwa kuwa kumsalimia ‘rafiki yake wa maisha’ na kiongozi wa taifa hilo, Kim Jong-un.

Akizungumza na waandishi wa habari katika uwanja wa ndege mjini hapa, Rodman alisema kuwa ‘anajaribu kuungua njia’ ya kueneza mchezo wa kikapu nchini humo.
 
“Ninajaribu kufungua njia na ndiyo maana ninaelekea nchini humo,” alisema nyota huyo wa kikapu ambaye alianzisha urafiki na Kim Jong-un mwaka 2013 baada ya safari yake ya kwanza nchini humo.
 
Kwa upande wao, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Marekani, ilieleza kwamba wanafahamu juu ya safari ya nyota huyo na kuongeza kwamba anasafiri kama raia wa kawaida na kumtakia heri na fanaka kwenye safari yake.
 
“Tunafahamu kuhusu safari ya Rodman (Dennis) na anasafiri kama raia yeyote wa kawaida lakini tumewaonya Wamarekani kuhusu kusafiri kwenda Korea Kaskazini. Hilo ni kwa usalama wao,” alisema Thomas Shannon ambaye ni ofisa wa juu kwenye wizara hiyo.

No comments