MWAMBUSI:MECHI YA TOTO AFRICANS ITAKUWA NGUMU KWETU

Kocha msaidizi wa Yanga SC, Juma
Mwambusi ameizungumzia mechi yao ya kesho dhidi ya Toto Africa kama
mechi ngumu na yenye ushindani mkubwa kutokana hali waliyonayo wapinzani
wao.
Mwambusi ametanabaisha wao kama
benchi la ufundi wameiandaa vyema timu yao kucheza kwa ushindani ili
washinde mechi hiyo na kujiweka katika mazingira mazuri ya kubeba
ubingwa wa ligi kuu.
Angalizo kwao ni ushindani dhidi
ya Toto Africa ambao wanahitaji alama tatu ili wasishuke daraja na
uchovu ( fatigue ) wa wachezaji wao kwa kucheza mechi mfululizo.
” tunatambua Toto kesho watacheza
kwa tahadhari kubwa ili kupata ushindi lakini tumewaandaa vyema
wachezaji kimbinu, kiufundi na kisaikolojia ili kushinda uchovu na
kucheza kwa moyo wote ” alieleza kocha huyo.
Mwambusi alikwenda mbali zaidi kwa
kusema anafahamu Toto Africa watakuja kwa mchezo wa kukamia hata
kuwashangaza wengi kwanini wanapambana sasa wasishuke daraja lakini wao
kama Yanga SC wanalifahamu hilo na wanazoefu nalo kama ilivyokuwa katika
mchezo wa jumamosi dhidi ya Mbeya City.
” tunafahamu watakuja kwa kukamia
dhidi yetu na tumejiandaa vyema kiufundi kwa hilo . Kushinda mchezo wa
kesho ni muhimu sana kwetu kuelekea ubingwa hivyo tahadhari zote
tumechukua ” alisema Mwambusi.
Yanga SC watacheza na Toto Africa
kesho uwanja wa Taifa majira ya saa 10:00 jioni ikiwa ni mechi yao ya 29
kuelekea mwishoni mwa msimu na alama zao 65 kileleni mwa ligi .
No comments