Header Ads

ad

Breaking News

DR. JOHN POMBE MAGUFULI ALITIKISA JIJI LA TANGA, WANANCHI WAFURIKA VIWANJA VYA TANGAMANO KUMSIKILIZA

1
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli akihutubia kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya Tangamano mjini Tanga leo, Dr. Magufuli amewaomba wananchi wa Tanga kumpigia kura za ndiyo ili aweze kufanya kazi na kulitumikia taifa, yeye kwake ni Kazi tu! kwani hata biblia inasema “Asiyefanya kazi na asile”.
Ameongeza kwamba mara atakapochaguliwa na kuongoza nchi ya Tanzania atahakikisha anafufua viwanda mbalimbali vilivyopo nchini na kujenga viwanda vipya vidogovidogo, vya kati na vikubwa ili kupunguza tatizo la ajira nchini lakini pia kukuza uchumi wa nchi kwa ujumla wake, Huku akiahidi kubana matumizi hovyo ya fedha za serikali ili ziweze kuwanufaisha wananchi wa hali ya chini ambao wanasumbuka na umasiki.
Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unatarajiwa kufanyika tarehe 25 Mwezi Oktoba Mwaka huu nchini kote ukishirikisha vyama mbalimbali vya kisiasa.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-TANGA)
2
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli akisisitiza jambo wakati akihutubia kwenye  mkutano wa kampeni zake uliofanyika kwenye viwanja vya Tangamano mjini Tanga.
3
Mwanamuziki nguli hapa nchini Diamond Platnumz akifanya vitu vyake jukwaani katika mkutano huo wa kampeni.
4
6
Mwanamuziki Ali Kiba akionyesha uwezo wake katika jukwaa wakati akitumbuiza kwenye mkutano wa kampeni wa CCM jijini Tanga.
8
Mzee Yusuf Makamba akizungumza neno katika mkutano huo na kuwafunda wananchi wa mkoa huo kutopoteza kura yao na kumpa Dr. John Pombe Magufuli wa CCM ili awatumikie.
9
Tangamano ikiwa imetapika umati wa wananchi wakimsikiliza Dr. John Pombe Magufuli.
10
Yamoto Band wakitifua jukwaa.
12
Mwanamuziki wa muziki wa taarab Mzee Yusuf naye akipagawisha wananchi katika mkutano huo.
13
Kada wa CCM na mwenyekiti wa Chama cha walemavu Ndugu Amon Mpanju akiwahutubia wananchi na kumpigia debe Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli.
15
Ummy Mwalimu akizunguza jambo katika mkutano huo.
16
Mwigulu Nchemba mgombea ubunge jimbo la Iramba Magharibi naye akatema cheche na kusema wapinzani ni watu wa dili tu, kila kitu dili.
17
Mgombea Ubunge jimbo la Bumbuli akimkaribisha Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli mkoani Tanga.
????????????????????????????????????
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli akiwapungia mikono wananchi wa mkoa wa Tanga mara baada ya mkutano kumalizika.
????????????????????????????????????
????????????????????????????????????
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM Ndugu Abdallah Bulembo akizungumza na mgombea ubunge wa jimbo la Bumbuli Mh. Januari Makamba kulia ni Mgombea ubunge wa jimbo la Iramba Magharibi Mwigulu Nchemba.
????????????????????????????????????
????????????????????????????????????
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli akihutubia kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika mjini Pangani leo.
????????????????????????????????????
Baadhi ya vijana waliokuja kumsikiliza Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli wakifuatilia hotuba yake huku wakiwa juu ya miti. 
????????????????????????????????????
\
Akina mama wakiwa wamejifunika na mabango yenye ujumbe wa kampeni ya Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli yanayosema “Magufuli Hapa Kazi Tu” wakiwa katika mkutano wa kampeni mjini Pangani. 
????????????????????????????????????
Vijana wakiwa katika miti wakimsikiliza Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli wakati akiwahutubia wananchi.
????????????????????????????????????
Hapa ni rangi za CCM tu.
????????????????????????????????????
Hii nyumba iliyopo kijiji cha Mkuza Mheza ni full mchanganyiko wao hawana bifu wanadhihirisha kwamba siasa siyo uadui kwa kuweka picha za wagombea wa CCM na UKAWA. 
????????????????????????????????????
Mzee huyu na Mgombea Udiwani wake kata ya Mkuza.
????????????????????????????????????
Hawa wanaonekana wamekunwa na sera za Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli 
????????????????????????????????????
Hapa wakapaza zaidi sauti zao wakisema “Wewe ni  Tingatinga letuuu!!
????????????????????????????????????
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli akimnadi Balozi Adadi Rajabu ambaye anagombea ubunge kupitia jimbo la Muheza.
????????????????????????????????????
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli akihutubia mkutano wa kampeni mjini Muheza.
????????????????????????????????????
 Dr. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Balozi Adadi Rajabu mgombea ubunge wa jimbo la Muheza.
????????????????????????????????????
Mchezea Chatu wa ngoma za utamaduni naye hakusita kufanya mambo yake katika mkutano wa kampeni wa CCM mjini Muheza.
????????????????????????????????????
Vijana wa Kabuku wakampokea Dr. John Pombe Magufuli.
????????????????????????????????????
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Mkata akiwa njiani kwenda Muheza, Pangani na Tanga mjini kwa ajili ya mikutano ya Kampeni ambapo aliwaambia atahakikisha anatatua tatizo la maji Mkata mara atakapochaguliwakuongoza nchi ya Tanzania.
????????????????????????????????????
Wananchi wakimsikiliza Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli huku kukiwa na madumu kwa ajili ya kuchotea maji Mkata ina tatizo kubwa la maji safi ya kunywa.

No comments