VITAMBUSHO KWA WAANDISHI WA MPIRA WA MIGUU
![]() |
Ofisa Habari TFF, Boniface Wambura |
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa vitambulisho vipya kwa waandishi wa habari za mpira wa miguu kwa ajili ya kuripoti mechi mbalimbali inayoziandaa na kuzisimamia.
Kila chombo cha habari kupitia Mhariri wake au Mhariri wa Michezo kinatakiwa kuwasilisha majina ya waandishi wake kwa barua maalumu ya ofisi pamoja na picha (soft copy) kwa ajili ya vitambulisho hivyo.
Orodha ya majina ya waandishi wakiwemo wapiga picha wanaoombewa vitambulisho hivyo iwekwe kwa umuhimu.
No comments