Header Ads

ad

Breaking News

Shabiki Leeds atupwa jela kwa kumpiga kofi kipa uwanjani


Aaron Cawley


LEEDS, England
SHABIKI wa timu ya Leeds United, ya England aliyemvamia kipa wa Sheffield Wednesday, Chris Kirkland, amefungwa wiki 16.

Aaron Cawley mwenye miaka 21, kutoka Cheltenham, alikiri kuvamia na kushambulia wakati wa mechi ya Sheffield Wednesday dhidi ya Leeds, iliyochezwa Ijumaa usiku katika uwanja wa nyumbani wa Sheffield.

 Cawley, aliyehudhuria mahakama ya Sheffield, alikamatwabaada ya kipa wa Wednesday, Kirkland kusukumwa kichwani wakati wa mechi hiyo iliyopigwa Hillsborough.

Kirkland, aliyewahi kuichezea timu ya England, alianguka chini baada ya tukio hilo, kufuatia bao la kusawazisha dakika ya 76.

Cawley alionekana kwenye kamera akikimbia kutoka upande wa mashabiki wa Leeds na kuingia uwanjani na kumsukuma Kirkland usoni, kabla ya kurejea tena kwa mashabiki wenzake. 

Macaulay alisema Cawley, aliwaambia maofisa kuwa, alilewa sana Ijumaa asubuhi, robo tatu ya pombe aina ya vodka, kabla ya kupanda treni kuelekea Sheffield.

Taarifa ya kwenye mtandao wa Leeds ilisema: Msemaji wa klabu alisema: "Tumefurahishwa kuona suala hili limeshughulikiwa na mahakama kwa haraka. Tunepata taarifa kuwa, amehukumiwa kwenda jela siki sita na kufungiwa miaka mitano.

No comments