Header Ads

ad

Breaking News

61 WASHUHUDIA MECHI YA AFRICAN LYON v POLISI MORO

Watazamaji 61 ndiyo waliokata tiketi kushuhudia mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya African Lyon na Polisi Moro iliyofanyika jana (Septemba 19 mwaka huu) Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.

Mapato yaliyopatikana katika mechi hiyo ambapo viingilio vilikuwa sh. 3,000 na sh. 5,000 ni sh. 185,000. Mgawo ulikuwa kama ifuatavyo; kila timu sh. 20,287.91, asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 27,457.62 na tiketi sh. 89,916.

Kamati ya Ligi sh. 6,762.63, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 4,057.58, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 2,703.05, gharama za mchezo sh. 6,762.63 na uwanja sh. 6,762.63.

No comments