Header Ads

ad

Breaking News

DSTV yapunguza gharama za kulipa


Barbara Kambogi, Meneja Uhusiano MultiChoice Tanzania

KATIKA  kuhakikisha DSTV inawakosha wapenzi wake katika matangazo yake ya moja kwa moja ya mpira wa miguu wamepungaza gharama za kulipia ili kuwapa fursa wadau wa soka kutumia king’amuzi hicho.

King’amuzi hicho cha DSTV kupitia kituo chake chake SuperSport ndio kituo pekee kitakachoonesha ligi kuu ya England, Hispania ‘La liga’, Italia Seria A, Ujerumani ‘Bundesliga’.

Mashindano mengine ambayo huoneshwa katika kituo cha SuperSports ni Ligi ya Klabu Bingwa na Mataifa ya Ulaya.

Kwa upande wa Afrika, Super Sports inaonesha ligi ya Afrika ya Kusini, Kenya, Uganda, Nigeria, Angola, Ghana, Zambia na mashindano ya yanayosimamiwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF).

Hata hivyo, DSTV imeendelea kuonesha mechi za Kombe la Dunia za wanawake  wenye miaka chini ya 20.

Super Spots kupitia king’amuzi chake cha DSTV, wamekuwa wakirusha matangazo ya mechi moja kwa moja zaidi ya mechi 1,400 kwa mwaka.

Baadhi ya vipindi ambavyo vitakuwa vikirusha matangazo hayo kuchambua soka ni Monday Night Football, EPL TV – Fan Zone, La Liga Highlights Show,  Simba Super Soccer, Soccer Africa, Mpira Zambia na Naija.

No comments