Header Ads

ad

Breaking News

Wanyange 15 wajitokeza Sinza


Miss Sinza
Na Mwandishi Wetu
WANYANGE 15 wamejitokeza  kuwania taji la Mrembo wa Sinza “Redds Miss Sinza 2012” yaliyopangwa kufanyika julai 13 kwenye ukumbi wa Mawela social (Ten Star  Lounge) uliopo karibu na hotel ya Vatican City.

Mratibu wa mashindano hayo, Majuto Omary wa kampuni ya Calapy Entertainment, aliwataja warembo hao ni Mariam Miraji, Naima Mohamed, Lulu Ambonela, Maria John, Eva Mushi na Vailet John.

Wengine ni Esther Mussa, Christina Samwel, Nahma Said, Shadya Ali, Aisha Ramadhan, Nancy Musharuzi, Brigitter Alfred na Merina Mushi.

Omary alisema kuwa, warembo hao wapo kambini chini ya mwalimu wao, Mwajabu Juma, ambaye kwa sasa anashikilia taji la Miss Tanzania Top Model.

 Alisema kuwa, mazoezi ya warembo hao yanafanyika kwenye ukumbi wa mashindano hayo, Mawela social kuanzia saa 8.30 mchana.

“Warembo wamepania kufanya kitu cha kihistoria siku ya mashindano na hii inatokana na ukweli kuwa, wamejiandaa vilivyo na kwa sasa wanamalizia tu baadhi ya vitu vidogo vidogo vya mashindano hayo, alisema Majuto.

Alisema lengo la mashindano ya mwaka huu ni kutwaa taji la Redds Miss Tanzania, mbali ya taji la Kanda ya Kinondoni katika shindano hilo lililodhaminiwa na Redds Premium Cold, Dodoma Wine na Kidoti Fashion.
Wadhamini wengine ni Clouds Entertainment, sufianimafoto.blogspot.com, Lady Pepeta na flexi P, Fredito Entertainment, Screen Masters, Brake  Point na Jackz Cosmetics Kinondoni.

“Tuna warembo moto wa kuotea mbali ambao kwa sasa wameonesha kupania kufanya kile ambacho kinachosubiliwa na wadau wa urembo wa mitaa ya Sinza na vitongoji vyake, hii inatokana na ukweli kuwa,  mashindano haya ni ya mwisho kwa upande wa vitongoji jijini,” alisema.
Miss Sinza

No comments