Header Ads

ad

Breaking News

Terry azidishiwa kibano UEFA



LONDON, England
NOHODHA wa timu ya ya soka ya Chelsea, John Terry, ameongezewa adhabu ya kukosa mechi mbili za ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, baada ya kutolewa nje kwa kadi nyekundu dhidi ya Barcelona, katika mchezo wa nusu fainali ya michuano hiyo.

Terry alioneshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja baada ya kumpiga kwa goti beki wa Barcelona, Alexis Sanchez, wakati wa mechi ya pili ya marudiano, aliikosa mechi ya fainali ya michuano hiyo iliyowapa kombe.  
UEFA iliamua kumfungia Terry mwechi tatu kwa mchezo mbaya dhidi ya mchezaji huyo, ingawa mechi ya fainali iliyochezwa Uwanja wa Allianz Arena mjini Munich itahesabiwa.
Kwa hiyo, atazikosa mechi za kuwania kombe la Ulaya kwa klabu dhidi ya Atletico Madrid, na mechi ya kwanza ya hatua ya makundi ya ligi ya Ulaya.
"Bodi ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Ulaya (UEFA) , limemsimamisha  mchezaji wa Chelsea FC, John Terry mechbi tatu za michuano hiyo," taarifa ilisomeka. "Kwa mchezaji huyo hakushiriki mechi ya fainali dhidi ya Bayern Munich Mei 19, tayari ametumikia mechi moja.
"Mechi mbili zilizobaki, atatumikia michuano ya klabu ya UEFA ambayo timu yake itashiriki. Rufani inawezekana ikawasilishwa siku tatu tangu itangazwe iwe na sababu maalum."

No comments