Header Ads

ad

Breaking News

Rodgers apata ulaji Liverpool, arithi mikoba ya Kenny Dalglish



LIVERPOOL, England
KOCHA mpya wa timu ya Liverpool, Brendan Rodgers, amesema ataanza mipango yake kwa kuijenga timu hiyo kwa ajili ya ligi ya England, baada ya kukabidhiwa mikoba na kuwa kocha wa 18 kuifundisha timu hiyo.

Rodgers alitakiwa kuwasili Anfield jana, baada ya makubalino na klabu yake ya zamani ya Swansea City, na muda mfupi akaweka wazi mipaango yake hiyo.
"Hii ni kazi ya muda mrefu," alisema Rodgers. "Ninataka kusimamia taratibu za klabu, soka la kushambulia na nidhamu.

"Inawezekana ikawa miaka 20 imepita tangu itwae ubingwa, tuwa wazi, hatutakuwa tayari sasa, lakini, mipango inaanza leo."

Rodgers alisema amefurahi kuwa kocha wa pili kutoka Ireland kuifundisha Liverpool,  na kwamba, awali aligoma kuhojiwa, lakini baada ya kuthibitishwa, ikajulikana kuwa, ni chaguo la kwanza Liverpool , ambapo haikuwa vigumu kwake, kuondoka Swansea.

"Siku nyingi nilikuwa nikisema, nitaondoka Swansea na kutua klabu kubwa, lakini nilipenda kuwa namba moja," alisema. "Kwa wakati huu, nilikuwa sehemu ya wanaobaki Swansea, lakini iliibuka tena na kuwa wa kwanza kutaikiwa.

"Mara nilipojua nimekuwa wa kwanza kusakwa, nilijiuzulu na ilikuwa rahisi."
Rodgers mwenye miaka 39, lakini alikanusha taarifa za kwamba, ametwaa kiti hicho akiwa na uzoefu mdogo, lakini alitoa mfano kwa mtangulizi wake, Kenny Dalglish, aliyeanza kufuundisha akiwa kocha mchezaji na kufanikiwa kutwaa ubingwa na Kombe la FA. 

"Mimi ni kijana kwa umri, lakini nina uzoefu wa mechi nyingi," alisema. "Soka ni soka,  wanataka kujifunza na wanataka kuelimika, na ndicho nilichokifanya katika majukumu yangu."

Mwenyekiti wa Liverpool , Tom Werner, aliyemtangaza  Rodgers kwa waandishi wa habari, ualielezea uzoefu wake uliowafanya wampe mkataba kocha huyo wa zamani wa Reading.

No comments