Header Ads

ad

Breaking News

Simba kumekucha Chang’ombe


Simba
MABINGWA wa soka Tanzania Bara, Simba SC, leo wanatarajia kuanza rasmi mazoezi yake katika Uwanja wa Sigara Chang’ombe jijini Dar es Salaam,  wakiwa wamekamilika.
Kikosi hicho kinatarajia kukamilika leo  baada ya wachezaji waliopewa likizo baada ya kuzitumikia timu zao za taifa, kuwasili katika kikosi hicho.
Wachezaji wanaotarajiwa kuanza mazoezi leo ni nahodha Juma Kaseja, Mwinyi Kazimoto, Amir Maftah, Nassor Said, Haruna Moshi ‘Boban’ na Juma Nyosso waliokuwa katika kikosi cha Taifa Stars.
Kwa upande wa wachezaji  waliosajiliwa msimu huu ni Kanu Mbiyavanga kutoka DR Congo, Salum Kinje aliyetokea AFC Leopard ya Kenya, beki Masombo Lino kutoka DC Motema Pembe ya DRC na kiungo Mussa Mudde kutoka Sofapaka.
Wachezaji ambao wamemaliza mkataba wao ni Ally Mustafa, Derick Walulya, Gervais Kago na Juma Jabu, huku  Rajabu Isihaka, Salum Machaku, Haruna Shamte na Shija Mkina wakitolewa kwa mkopo.
Kikosi hicho kitaanza kunolewa na Kocha Milovan Cirkovic baada ya kuwasili nchini akitokea kwao Serbia likizo.
Mashabiki wa timu hiyo waliohudhuria mazoezi ya jana, walisikika wakisema kuwa, ‘mashine’ zao zote zitaanza mazoezi leo, hivyo kocha atakuwa na kazi kubwa ya kuangalia wachezaji atakaowatumia katika kombe la Kagame.
Mazoezi hayo ni kwa ajili ya maandalizi ya kombe la Kagame ambalo linatarajiwa kuanza Julai 14, mwaka huu. Yanga ni mabingwa watetezi wa Kombe hilo.
Cirkovic, leo ataanza rasmi kuinoa timu hiyo huku ikiwa imejaa nyota wake wote wapya na wa zamani ambao walipewa likizo baada ya kuitumikia timu ya taifa.

No comments