Header Ads

ad

Breaking News

Beckham aikosa michuano ya Olimpiki


David Beckham
LONDON, England
NDOTO za nyota wa zamani wa soka nchini Uingereza, David Beckham, za kucheza michuano ya Olimpiki mwaka huu, zimepotea, baada ya mchezaji huyo kuachwa kwenye kikosi kitakachocheza michuano hiyo itakayofanyika jijini London.

Kocha Stuart Pearce, amemwacha kiungo huyo wa Los Angeles Galaxy, katika kikosi chake kitakachocheza michuano itakayoshirikisha timu 16, alikataa kumpa nafasi mchezaji huyo mwenye miaka 37, katika idadi ya wachezaji watatu waliozidi miaka 23.

"Kila mmoja anajua jinsi nilivyokuwa nikiichezea timu yangu, kwa hiyo wangenijumuisha kama kunienzi katika kikosi cha GB," Beckham alisema katika taarifa yake iliyotolewa na mwakilishi wake.

"Kwa kawaida, imenikatisha tama, lakini haitakuwa na mashabiki wengi kama ambavyo ningekuwemo mimi na ninawapenda, nina matumaini watatwaa medali ya dhahabu."

Beckham alikuwa sambamba na Sebastian Coe kushawishi Kamati ya Olimpiki Duniani kuipeleka michuano hiyo jijini London, ikiwa ni mara ya tatu kuandaa tangu mwaka 2005.

No comments